• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

“Kituo Hiki sasa kina hadhi ya Hospitali ya Wilaya”Mhe. Samia Suluhu Hassan!

Posted on: December 14th, 2019

Mhe. Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amefanya ziara Katika kisiwa cha Ukara na kuzindua Kituo cha Afya Bwisya kilichojengwa kwa gharama ya Billioni 1.3 fedha ambayo katika maeneo mengine hutolewa kujenga Hospitali ya Wilaya. “Nasema Ukerewe Oyee kwa sababu mtakua na hospitali mbili za Wilaya, moja Nansio na nyingne Bwisya” Mhe Samia Suluhu Hassan.

Ameagiza Naibu waziri wa  Wizara ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mhe. Mwita Waitara (MB) na Naibu katibu Mkuu Wizara ya Afya Doroth Gwajima kwenda kupitia vigezo vyote na hatua zote na Kituo cha Afya Bwisya kuwa Hospitali ya Wilaya.

Makamu wa Rais Ametoa Pole kwa wote waliopoteza ndugu, jamaa na marafiki Katika Ajali ya kuzama kwa Kivuko cha MV. Nyerere kilichotokea septemba 20,2018. Amewapongeza Watanzania wote waliochanga wakati wa maafa.

Makamu wa Rais ametoa Salamu za Pongezi kutoka kwa Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua nzuri ya Ujenzi wa Kituo hiko na namna wananchi wanavyoendelea na shughuli za uzalishaji kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo kilimo.

Makamu wa Rais ametoa wito kwa Wana Ukara kuitunza Hospitali hii kwani ni Mali yao. Hivyo ni wajibu kuitunza kama Mali yao kwani serikali imeshafanya wajibu wake wa kuwajengea Hospitali.

Serikali inafahamu Upungufu wa watumishi hapa lakini Wizara ya Afya imeandaa list ya watumishi wote wanao hitajika Hapa Bwisya na wakisha hitimu wataletwa.

Awali Naibu Waziri OR TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara (MB) alieleza kuwa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Huduma ya X-ray itapatikana Bwisya.

Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Cornel Magembe ameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa kujali na ameendelea kwa kusisitiza kuwa ni furaha kama Kituo cha Afya Bwisya kitakua Hospitali ya Wilaya.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.