• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

Ufugaji Nyuki

KITENGO CHA UFUGAJI NYUKI

UTANGULIZI

Kitengo cha ufugaji nyuki ni moja ya vitengo sita vilivyopo Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe. kitengo cha ufugaji Nyuki ndicho chenye jukumu la kusimamia na kuhakikisha mazao ya Nyuki yanazalishwa kwa tija na kuwa njia mbadala ya kuongeza kipato na kukuza uchumi kwa wananchi  baada ya shughuli zitokanazo na kilimo na uvuvi ambazo ndio shughuli kuu katika visiwa hivi vya Ukerewe.

Kwa miaka mingi, shughuli ya kilimo imekuwa shughuli kuu yauzalishaji katika wilaya ya Ukerewe na Tanzania kwa ujumla, shughuli inayo ajili wastani wa asilimia 80 ya wananchi wote. Pamoja na uzalishaji wa mazao ya Nyuki kama asali na Nta, ufugaji wa Nyuki una mchango mkubwa katika uzalishaji na kufanikiwa kwa shughuli ya kilimo. Hii inatokana na mchango mkubwa wa uchavushaji unaofanywa na wadudu hawa kwa wastani wa asilimia 75 – 80 kutokana na taarifa za machapisho mbalimbali. Hivyo wilaya ya Ukerewe kwa kuona umuhimu wa wadudu hawa, imebaini kuwa ili kuboresha shughuli za kilimo pamoja na kuongeza aina tofauti ya mazao ni bora shughuli za kilimo zifanyike sambamba na ufugaji wa nyuki kwa lengo la kuinua ubora wa mazao ya kilimo, lakini pia mazao kama asali itokanayo na nyuki itatumika kama njia mbadala ya kuongeza kipato na lishe kwa watumiaji.

Mizinga ya nyuki imetundikwa katika miti kikundi cha TUMA kijiji cha Hamkoko

Mizinga ya nyuki ikiwa imetundikwa katika chanja kikundi cha TUMA Kijiji cha Hamkoko

SHUGHULI MBALIMBALI ZINAZOFANYIKA

Kuhamasisha ufugaji: shughuli kuu ya uchumi Wilaya ya Ukerewe ni Uvuvi. Shughuli nyingine ni kilimo, uhifadhi wa misitu na mifugo. Ufugaji Nyuki ulikuwa ukifanyika kwa baadhi ya kaya kwa sababu maalumu, aidha walina asali walikuwa na taratibu za kutafuta asali katika mapango na misitu ambako makundi ya Nyuki yalipatikana kwa urahisi. Ifinyu wa ardhi, kupanuka kwa shughuli za kilimo na makazi kulichangia kuhamisha na kupunguza mtawanyiko sawia wa makundi ya Nyuki katika maeneo mbalimbali wilayani. Changamoto hii na umuhimu wa mazao ya Nyuki imepelekea kitengo cha ufugaji Nyuki kwa kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo kama shirika la EMEDO kuwa na shughuli ya kuhamasisha ufugaji wa Nyuki na hasa kwa kutumia mbinu ya inayosisitiza ufugaji wa makundi mengi katika eneo dogo ili kukabiliana na changamoto ya ufinyu wa ardhi.

Baadhi ya wanakikundi cha Nakaligata katika kijiji cha Murutanga wakikamua asali 

Kuwezesha upatikanaji wa zana za ufugaji: Ufugaji Nyuki ni shughuli isiyohitaji matumizi makubwa ya nguvu na muda kama ilivyo katika shughuli za kilimo na uvuvi. Changamoto kubwa ni uwekezaji wa mwanzo hasa zana za ufugaji na ardhi. Kitengo kwa kushirikiana na wadau wengine wamerahisisha upatikanaji wa baadhi ya zana kama mizinga ya Nyuki. Kituo cha mafunzo ya Ufundi Bukongo na Kituo cha Ufundi cha walemavu pia Bukongo, hivi ni baadhi ya vituo vinavyotengeneza mizinga ya Nyuki kwa gharama nafuu na kutoa mafunzo bila malipo kwa mafundi wengine kutoka maeneo mbalimbali wilayani. Kwa wastani kata 19 kati ya kata 25 zilizopo Ukerewe kuna mafundi wa kutengeneza mizinga. Wadu wengine kama shirika la uhifadhi wa bonde wa ziwa victoria (LVEMP) na Rotary Club, wanatoa mchango mkubwa kuwezesha upatikanaji wa vifaa vya Ufugaji Nyuki.

Usafirishaji mizinga kwa wafugaji kata ya Muriti ufadhili wa mradi wa LVEMPII

Upatikanaji wa masoko: Ufugaji wa Nyuki unafanywa na wananchi katika mfumo wa vikundi na wafugaji binafsi. Wengi wao wanapatikana vijijini kuliko na ardhi na mazingira mazuri ya ufugaji. Pamoja na changamoto zingine, pia upatikanaji wa masoko ni changamoto nyingine kwao, kutokana na mazingira yanayopelekea kuminya wigo wa mawasiliano juu ya taarifa za masoko ya mazao ya Nyuki. Kitengo kwa kushirikiana na wafugaji hawa kimekuwa na wajibu wa kutafuta taarifa za masoko  na kuhakikisha kwamba mazao haya yanapata wanunuzi.

Huduma za ugani: Ili ilani ya uchaguzi ya CCM iweze kutekelezwa kwa ufasaha, ni wajibu wa Kitengo kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ili kuwezesha uzalishaji wa mazao ya nyuki yanayokidhi mahitaji ya chakula na biashara. Katika kufanikisha hitaji hili kitengo kinatoa na kuboresha huduma za ugani, hii ni pamoja na kuwashawishi wafugaji wajiunge katika vikundi vidogo vidogo  vyenye umoja na nguvu vya ujasiliamali ili waweze kupata tija katika uzalishaji. Wilaya ya Ukerewe ina jumla ya wafugaji 62 walio katika vikundi na wafugaji binafsi.

Kikundi cha BMU Bugula wakiadhimisha siku ya utundikaji mizinga

Changamoto kubwa inayowakabili wafugaji hawa ni upungufu mkubwa wa wataalamu wa ufugaji Nyuki, hali hii hukwaza upatikanaji wa huduma ya wataalamu kwa wakati na muda muafaka. Ili changamoto hii iweze kupata ufumbuzi ni halmashauri ya wilaya kupata kibali cha kuajiri maafisa ugani upande wa Nyuki na kuwaelekeza kwenda kuishi jirani na wafugaji ikiwa ni pamoja na kuwaborehea makazi na huduma ya usafiri utakao wawezesha kuwafikia wafugaji kwa wakati.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.