• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika

IJUE IDARA YA KILIMO UMWAGILIAJI NA USHIRIKA

UTANGULIZI

Idara ya Kilimo inaundwa na sehemu tatu ambazo ni Mazao, Umwagiliaji na Ushirika. Idara hii ndiyo ina jukumu la kuhakikisha Wilaya inazalisha mazao ya chakula na biashara kwa tija na kuwa na uhakika wa chakula kwa ajili ya wananchi wote kupitia shughuli za kilimo zinazosimamiwa na Idara kwa kusaidiana na wadau wengine wa Kilimo kutoka nje na ndani ya Wilaya

Kilimo ndicho maisha ya kila siku na uchumi kwa wananchi walio wengi kwa kila dakika inayopita. Kila mtu , kila mahali katika Wilaya na hata katika nchi nzima lazima aone, ashike na afanye kitu kinachohusianna na kilimo katika mtazamo chanya au mtazamo hasi. Hii inaelezea ni kwa nini kilimo ni muhimu na uti wa mgongo wa uchumi wetu kwani kilimo ndicho kinaajiri zaidi ya asilimia 80 ya watanzania na kiasi cha asilimia 92 cha wakazi wa wilaya ya Ukerewe ambaohutegemea kilimo.

SHUGHULI MBALIMBALI ZINAZOFANYIKA 

Mazao yalimwayo kwa wingi katika Wilaya ya Ukerewe yenye visiwa 38 japo visiwa 15 vinatumika kama maeneo ya uvuvi ni muhogo, viazi vitamu, mpunga, matunda aina ya machungwa, maembe, mananasi, mapapai, kahawa, migomba, mazao ya 


bustani na mazao ya jamii ya kunde kama vile maharage, njugu mawe na kunde. Mazao mengine yanayolimwa kwa kiasi kidogo ni mtama na rosella (choya). Mazao haya yanalimwa katika eneo la Ha.33, 765.5
Ardhi iliyopo ni ndogo kuruhusu kilimo cha kupumzisha mashamba. Kwa hali hiyo kilimo kinahitaji kifanyike kwa tija ili uzalishaji wa mazao uweze kukidhi mahitaji ya wananchi wote ambao kulingana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ni 347,145. Zao la alizeti linatiliwa mkazo badala ya zao la pamba ambalo katika
miaka ya 1970 lilikuwa zao maarufu la biashara ambalo lilikuwa linawapatia wakulima kipato. Lakini kutokana na upungufu wa ardhi hasa ukizingatia kuwa zao hili halitakiwi kuchanganywa na mazao mengine pamoja na kushuka kwa bei, zao hili lilionekana kutofanya vizuri.


Idara ya Kilimo ili iweze kutekeleza vyema ilani ya Uchaguzi ya CCM ni lazima ihakikishe inatekeleza majukumu mbalimbali ya msingi ili kuleta tija katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara, kuendeleza na kuboresha huduma za ugani ikiwa ni pamoja na kuwezesha wakulima kuwa na vyama vya ushirika vilivyo hai na vyenye nguvu ya mtaji. Aidha kuwawezesha wakulima kuunda vikundi ili waweze kuwa na umoja wenye nguvu katika kufikisha bidhaa zao katika masoko ya mazao yao. Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ina jumla ya Vyama Vya Ushirika 71 vilivyoandikishwa chini ya Sheria Na.6 ya mwaka 2013 ya Vyama Vya Ushirika. Idadi ya VICOBA vilivyopo ni 150. Vyama vilivyo vingi vinakabiliwa na matatizo mbalimbali ambayo yanapelekea vyama hivyo kutofanya vizuri. halmashauri inakabiliwa na upungufu wa wataalam 4 wa Ushirika kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji wa vyama hivyo ikiwa ni pamoja na kufanya ukaguzi wa mahesabu. Ili haya yaweze kufanyika kwa ufanisi Maafisa Ugani wanatakiwa kuboreshewa mazaingira yao ya kufanyia kazi. Maboresho hayo ni pamoja  na kupatiwa nyumba za kuishi katika maeneo yao na kuwezeshwa vyombo vya usafiri hususani pikipiki ili kuwawezesha kuwafikia wakulima kwa urahisi na kwa muda muafaka pale huduma za ugani zinapohitajika.

Pamoja na Serikali kutilia mkazo juu ya kilimo cha umwagiliaji wakulima bado wanategemea mvua katika kilimo. Hii ni kutokana na kutokamilika kwa miundo mbinu ya umwagiliaji katika skimu za Bugorola na Miyogwezi. Miradi hii imekwamakukamilika kutokana na ukosefu wa fedha licha ya Ofisi hiyo ya Umwagiliaji

 Kibanio (Head Work) katika skimu ya umwagiliaji Miyogwezi

Kanda ya Ziwa kuomba fedha mara kwa mara kutoka Serikalini kwa ajili ya kukamilisha miradi. Hata hivyo jitihada zinaendelea ambapo Halmashauri katika Bajeti ya Mwaka 2017/2018 imetenga jumla ya Tsh. 354,141,458.40 kwa ajili ya kukamilimisha mradi wa Bugorola.

Mashine ya kusukuma maji katika skimu ya umwagiliaji Bugorola

Upatikanaji wa takwimu sahihi za utekelezaji wa shughuli za kilimo  kwa wadau wa kilimo ni muhimu sana kwa ajili ya kuandaa sera na miongozo mbalimbali. Ili kuhakikisha suala hili linatekelezwa kwa ufanisi Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) limesaidia kuandaa mfumo wa utoaji wa takwimu za kilimo kutoka ngazi ya Kata hadi Taifa kwa kutumia “internet” yaani Agricultural Routine Data System (ARDS-Web Portal). Mfumo huu unawezesha wadau mbalimbali wa maendeleo nchini kupata takwimu za kilimo kutoka maeneo mbalimbali kwa urahisi zaidi tofauti na ilivyokuwa hapo awali. Changamoto kubwa tuliyonayo ni upungufu mkubwa wa maafisa ugani ngazi ya kijiji na kata, hivyo kupelekea baadhi ya maafisa ugani kuhudumia kata zaidi ya moja. Vyombo vya usafiri kwa maafisa ugani pia ni tatizo ili kuwafikia wakulima kwa wakati katika maeneo yao ya kilimo. Kuwepo kwa kituo kikubwa cha rasilimali za wakulima na wafugaji katika kata ya Bukindo kumesaidia wakulima na wafugaji kupata maarifa juu ya kilimo cha mazao,ufugaji bora wa mifugo, uvuvi na ufugaji bora wa nyuki kupitia vitabu mbalimbali vilivyonunuliwa kwa fedha za DADP. Aidha kituo hiki kina ukumbi mzuri kwa ajili ya mikutano, warsha na mafunzo. Kutokana na ukosefu wa maeneo kwa ajili ya kujenga vituo vya wakulima wilaya iliamua kuwa na kituo kimoja kikubwa ambacho kitahudumia wakulima wote wilayani.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.