• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

JAMII YAPEWA SEMINA ELEKEZI KUHUSU SARATANI YA MATITI

Posted on: September 29th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la jhpiego linalojishughulisha na masuala ya afya ya mama na mtoto kupitia mradi wa "PFIZER BREAST CANCER "

wametoa semina elekezi kwa viongozi wa dini,watendaji wa kata, wahudumu wa afya ngazi ya jamii na wahanga wa saratani ya matiti juu ya ugonjwa huo na namna ya kuepukana nao.

Akifungua semina hiyo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo ndugu Chinchibera Wanchoke amesema bado jamii ya Ukerewe inahitaji kupata elimu ya kutosha juu ya saratani ya matiti kufuatia takwimu mbalimbali zitatolewa zikionyesha maeneo mengi ya ukanda wa ziwa kuwa waathirika wakuu.

Akitoa mafunzo hayo Dkt.Matobera Mugini wa hospitali ya Nansio amesema saratani ya matiti ni ugonjwa unaotokana na chembechembe hai katika matiti zinazokuwa na kugawanyika bila udhibiti maalum .

Amezitaja baadhi ya dalili za ugonjwa huo kuwa ni pamoja na uvimbe , mabadiliko ya ngozi kwenye matiti na chuchu huku akiwataka kina mama kuwahi hospitali punde wanapoona mabadiliko hayo.

Aidha Dkt.Matobera ameainisha namna ya kujilinda na saratani hiyo kwa kuwataka wanawake kujichunguza wenyewe, kuzingatia uzito sahihi wa mwili, kufanya mazoezi, kupunguza unywaji wa pombe, kuepuka matumizi ya sigara na kunyonyesha kwa kuzingatia ushauri wa wataalam wa afya.

Nae Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo Dkt.Charles Mkombe amesema wagonjwa wengi wanakwenda hospitali kwa kuchelewa hali inakuwa mbaya na kunakuwa hakuna namna ya kumsaidia mgonjwa zaidi ya kumpatia dawa za kupunguza maumivu na kumtia moyo na kuwataka kina mama kuwahi hospitali punde wanapoona mabadiliko yoyote kwenye matiti yao.

Lucas Lyimo ni Afisa takwimu na ufuatiliaji wa shirika la jhpiego yeye anasema shirika hilo lipo tayari kusaidia jamii kwa kuendelea kubuni miradi ya afya inayogusa jamii moja kwa moja na kutoa uelewa.

Akihitimisha semina hiyo Dkt.Matobera ameiasa jamii ya Ukerewe hasa kina mama ambao ndio waathirika wakuu wa saratani ya matiti kuachana na imani potofu za kishirikina juu ya ugonjwa huo na mgonjwa kujikita zaidi na matibabu ya kienyeji na baadae kwenda hospitali wakiwa wamechelewa na madhara yameshakuwa makubwa.

















Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI 2025 September 03, 2025
  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • JAMII YAPEWA SEMINA ELEKEZI KUHUSU SARATANI YA MATITI

    September 29, 2025
  • ULINZI WA TAIFA LETU NI JUKUMU LA KILA MTANZANIA

    September 26, 2025
  • JAMII UKEREWE YAASWA KUCHANGIA CHAKULA SHULENI

    September 25, 2025
  • WANANCHI WATAKIWA KUIMARISHA AMANI NA MSHIKAMANO

    September 24, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.