• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

Posted on: January 8th, 2026

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ukerewe Ndugu Vincent Augustino Mbua ameongoza kikao kazi cha maandalizi ya mapokezi ya wanafunzi kuanza darasa la awali, darasa la kwanza na waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza kilichohusisha Maafisa elimu kata na watendaji wa kata wote katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri.

Akizungumza katika kikao hicho Ndugu Mbua ametoa maelekezo kwa maafisa na watendaji hao kuhakikisha wanafunzi wote wanajiunga na masomo na kusiwepo sababu yoyote ya kuwazuia .

"... Hilo ni agizo la waziri wa nchi ofisi ya waziri Mkuu - TAMISEMI Mhe.Prof.Riziki S.  Shemdoe tuhakikishe wanafunzi waliopangwa kwenye shule zetu wote wanajiunga na kidato cha kwanza  mwanafunzi asizuiliwe kwa sababu yoyote ile hata kama hana sare za shule, simamieni zoezi la uandikishwaji kwa wanafunzi ..." 

Nae Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Mhe. Ramadhan S. Mazige amewataka maafisa na watendaji hao kuyafanyia kazi na kutekeleza makubaliano ya kikao hicho huku akiwasihi kuwa mstari wa mbele katika kusimamia ukusanyaji  wa mapato ya Halmashauri katika maeneo yao.

Katika kikao hicho Maafisa hao wamethibitisha utoshelevu wa miundo mbinu tayari kuwapokea wanafunzi wa elimu ya awali, darasa la kwanza na kidato cha kwanza huku wakithibitisha kuendelea kwa mchakato wa uandikishaji na ukamilishaji baadhi ya miundo mbinu ambayo inatarajiwa kukamilika punde.

Nae Kaimu afisa elimu msingi Rasuli Amir Hamis amewasisitiza maafisa hao kutoa maelekezo kwa wakuu wa shule katika kusimamia ukamilifu wa miundombinu kama madawati ili watoto wote wapate mahali pa kukaa.

Kwa upande wake Afisa elimu taaluma msingi Joseph Gatahwa Max  amewakumbusha maafisa hao kuzingatia mkakati wa ufundishaji ili kukuza taaluma na ufaulu wa wanafunzi hasa katika mitihani ya upimaji kwa watahiniwa.

Akiwasilisha taarifa ya hali miundombinu Afisa elimu kata ya Nansio Salome Maseta ameiomba serikali kuendelea kukarabati majengo yaliyochakaa na kumalizia maboma ili kupunguza adha ya mlundikano kwa wanafunzi.


















Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA USAILI December 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • WANAVIKUNDI VYA MIKOPO 10%WAASWA KUWA NA NDOTO KUENDESHA MIRADI MIKUBWA

    January 06, 2026
  • DKT.BASHIRU AWAASA WANANCHI KUTHAMINI UVUVI NA MIFUGO

    December 29, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.