• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

WANAVIKUNDI VYA MIKOPO 10%WAASWA KUWA NA NDOTO KUENDESHA MIRADI MIKUBWA

Posted on: January 6th, 2026

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Mhe.Ramadhan Salum Mazige ameviasa vikundi vya mikopo ya 10% (4% wanawake ,4% vijana,2% watu wenye ulemavu) inayotolewa Halmashauri kuwa na ndoto ya kuendesha miradi mikubwa zaidi kwa lengo la kujiinua kiuchumi kupitia shughuli na miradi mbalimbali inayoibuliwa na wanakikundi wenyewe . 

Akizungumza wakati akifungua mafunzo ya kujengea uwezo vikundi 18 vinavyotarajia kunufaika na mikopo hiyo juu ya usimamizi na matumizi bora ya fedha Mhe.Mazige amesema ni muhimu wahusika kupata elimu kabla ya kupewa mikopo ili kujenga uelewa wa pamoja ambao utawaondoa katika fikra za kuwaza miradi midogo midogo na kuwawezesha kuwaza miradi mikubwa yenye tija wakisimamiwa na wataalam wa maendeleo ya jamii.

"..mkope kwa malengo na utekelezaji usiende nje mpango ili muweze kurejesha vizuri na wengine waweze kunufaika na kufanya zoezi la rukopeshaji kuwa endelevu.."

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Ndugu Vincent Augustino Mbua amesema ataendelea kutenga fedha za mikopo hiyo kwa kufuata miongozo na maelekezo ya serikali.

Ndugu Mbua ameongeza kuwa fedha za mikopo ya 10% ni za serikali kwa manufaa ya wananchi wote huku akisisitiza fedha hizo sio za bure zinapaswa kurejeshwa na kuwataka wazingatie matumizi sahihi.

Wanchoke Nchichibela ni Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii Wilaya ya Ukerewe amesema mikopo hiyo haina ubaguzi bali inatolewa kwa wanaotimiza vigezo na kuwasihi wanavikundi kutoa taarifa sahihi kuepuka changamoto ya udanganyifu.

Jonas Mapesa na Siwema Malima ni miongoni mwa wanavikundi vya MASU group Kagera SIMATARANDO women group Bukongo waliopata mafunzo wanaipongeza Halmashauri kwa kuwaandalia mafunzo hayo ambayo yamewakumbusha majukumu, wajibu na haki zao katika kuhakikisha wanafanikiwa kupitia mikopo hiyo ya 10%.


















Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA USAILI December 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • WANAVIKUNDI VYA MIKOPO 10%WAASWA KUWA NA NDOTO KUENDESHA MIRADI MIKUBWA

    January 06, 2026
  • DKT.BASHIRU AWAASA WANANCHI KUTHAMINI UVUVI NA MIFUGO

    December 29, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.