• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

Maendeleo ya Jamii

KUHUSU IDARA YA MAENDELEO YA JAMII

UTANGULIZI.

Idara ya Maendeleo ya Jamii ni miongoni mwa Idara 13 katika Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe. Idara ina jumla ya watumishi 13 wakiwemo Maafisa Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Afisa Vijana .Wilaya ya Ukerewe ina kata 25 kati ya 7 ndio zina Maafisa Maendeleo ya Jamii.

SHUGHULI ZA IDARA.

  • Kuelimisha jamii zitambue kuwa rasilimali za kuleta maendeleo ziko ndani ya jamii zenyewe na kwamba wanao uwezo wa kuzibaini na kuzitumia kwa ajili ya maendeleo yao badala ya kusubiri serikali au wadau wengine wa Maendeleo. 
  • Kuhakikisha kuwa mipango na shughuli zote zinazofanywa na jamii ziwe zenye kuleta maendeleo yenye kuzingatia jinsia. 
  • Kuhamasisha na kutambua vikundi vya wanawake wajasiriamali na kutoa mafunzo/ elimu ya ujasiriamali. 
  • Idara inatoa mikopo kwa wanawake kupitia vikundi vya watu watano. 
  • Idara inatoa elimu ya ujasiriamali na ubunifu mbalimbali kwa vikundi vya vijana. 
  • Idara inaratibu shughuli za maendeleo ya vijana na kuwapatia mikopo.
  •  Idara inatoa elimu ya stadi za maisha na afya ya uzazi kwa vijana.
  •  Kutembelea na kuvitambua vituo vya kulelea watoto pamoja na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wasimamizi wa vituo hivyo. 
  • Kujenga uelewa kwa jamii kuhusu masuala ya jinsia na maendeleo kupitia wataalamu wa Idara. 
  • Utambuzi wa watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi kwa kushirikiana na asasi mbalimbali. 
  • Kutoa mikopo kwa wanawake na vijana na kuwapatia mafunzo juu ya mbinu za kuendesha biashara na kuzingatia masharti ya mikopo bila itikadi wala siasa.
  •  Kutoa elimu ya lishe bora kwa watoto wadogo na malezi yanayostahili na kupiga vita ajira ya watoto. 
  • Kuhamasisha wanawake kushiriki katika nafasi mbalimbali zenye kutoa maamuzi ili jamii itambue uwezo wa wanawake. 
  • Kufanya ufatiliaji  wa  mara kwa mara kwa vikundi vya  uzalishaji mali vya vijana na wanawake.
  •  Kuhamasisha uanzishwaji wa vikundi vya kuweka na kukopa kwa kushirikiana na Idara ya Ushirika.
  •  Kushirikiana na wadau wa maendeleo ili kuwa na nguvu ya pamoja katika kuleta maendeleo na usawa wa kijinsia. 
  • Kusajili CBO, FBO’s, na vikundi vya uzalishaji mali. 
  • Idara inaratibu shughuli zinazoendeshwa na Mashirika ya hiyari katika Halmashauri kwa kutoa ushauri na miongozo ya namna ya kuendesha shughuli zao pamoja na kuwaunganisha na wadau wengine wa maendeleo.
  •  Kusajili vyombo vya watumiaji maji (COWSO), na kuhamasisha jamii kujiunga na kusajili vyombo vyao. 

Idara inafanya kazi kwa kushirikiana na idara zingine ili kuleta maendeleo kwa wananchi.

 

 SHUGHULI MBALIMBALI KWA UFAFANUZI NI KAMA IFUATAVYO.

 A: UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE KUANZIA MWAKA 2006/2007 – 2009/2010 na 2014/15

Jumla ya 58 vikudi  vilivyo kopeshwa  kutoka katika Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake kutoka.  mwaka 2006/07, vikundi 12, 2008/2009 vikundi 15  2009/10 vikundi 18  na  2014/15 vikundi 13 vyenye jumla ya wanawake 290

Jumla ya Mikopo iliyotolewa kwa vikundi 58  ni Tsh. 31,700,000/= toka mwaka 2006/07 hadi 2014/15.

B: VIJANA 

Jumla ya vikundi vya vijana ni 3 ambao  wamepatiwa  kiasi cha fedha 10,000,000/=na wanajishughulisha na ufugaji wa kuku  na nguruwe pamoja na upandaji miti.Pia kuna fedha ambazo zimepokelewa kiasi cha tsh 4,750,000 zimepokelewa kutoka wizara yenye dhamana ya maendeleo ya vijana  kwa ajili ya kukopesha vikundi 3, utaratibu wa kuwakabidhi fedha  unafanyika.

Mafunzo  ya ujuzi yanatolewa kwa Vijana 87  kati ya hao  ke 52 na me 35  katika   fani mbalimbali  kama vile  ufundi umeme wa majumbani,,matengenezo ya pikipiki ,saluni, kudarizi,matengenezo ya simu , kushona nguo, upikaji wa vyakula, kuchomelea vyuma(welding), uashi, uwekaji wa vigae majumbani na kilimo cha bustani kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali Swiss contact chini ya mpango wa U Learn. Vijana hawa wamewezeshwa elimu ya ujasiriamali, stadi za maisha, uongozi wa vikundi na namna ya kujikinga na maambukizo ya UKIMWI

C: UKIMWI.

Idara inashirikiana na Idara ya Afya katika mapambano dhidi ya UKIMWI.

Maeneo ambayo idara ya Maendeleo ya Jamii imejikita zaidi ni:

  • Kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi ya UKIMWI.
  • Kutoa huduma ya misaada ya Chakula chenye viinilishe na fedha kwa vikundi vya watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI.
  • Kutoa msaada wa kuwalipia karo na sare za shule watoto yatima na waishio katika mazingira hatarishi.
  • Kuimarisha kamati za kudhibiti UKIMWI za ngazi zote.
  • Kufanya kampeni za  kuzuia maambukizi ya UKIMWI kupitia michezo na upimaji wa hiyari.
  • Kuunda klabu mbalimbali za vijana walio mashuleni na walio nje ya shule ili kujikinga na maambukizi ya UKIMWI.

D: USTAWI WA JAMII.

Idara ya maendeleo ya jamii, kupitia kitengo cha ustawi wa jamii inafanya shughuli zifuatazo.

  • Kufanya utambuzi wa watoto yatima na waishio katika mazingira hatarishi kupitia wasaidizi wa ustawi wa jamii walio katika vijiji.
  • Kutoa msaada kwa watoto yatima na waishio katika mazingira hatarishi kwa  kushirikiana   na Asasi zinazojihusisha na watoto.
  • Kutoa suluhu ya migogoro ya ndoa na kuwasilisha mahakamani migogoro inayoshindikana kwa ajili ya utatuzi zaidi.
  • Kusaidia watu walio katika makundi maalum kama vile Wazee, walemavu, watoto na Wanawake.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.