Timu ya menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ikiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo ndugu Goodluck Mtigandi imetembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyokubalika.
Sambamba na hayo timu hiyo imejadili na kutoa ufumbuzi wa changamoto zinazoonekana kuwa kikwazo cha ukamilishaji wa baadhi ya miradi.
Miradi iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri kwa fedha kutoka serikali kuu, mradi wa hoteli katika kata ya Nansio unaojengwa kwa fedha za mapato ya ndani sambamba ujenzi wa vyumba vya maduka 42 awamu ya tatu vilivyopo soko kuu la Nansio ndani ya kata ya Kagera ambapo Halmashauri ilipokea jumla ya shilingi milioni 300 kutoka serikali kuu.
Miradi yote inaendelea vizuri,kazi zinaendelea .
Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.