• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

“ACHENI MIVUTANO TUIJENGE IRUGWA”

Posted on: December 4th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Kanali Denis Mwila akiwa ameambatana na kamati ya Ulinzi na Usalama na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Leo wametembelea kisiwa cha Irugwa katika kata hiyo yenye vijiji viwili vya Sambi na Nabweko dhumuni likiwa ni kukagua Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika kata hiyo iliyopo kisiwani ambayo ni takribani zaidi ya saa sita kufika kutoka Nansio.

Miradi iliyotembelewa ni pamoja na Shule ya Msingi Buluza iliyopewa Tsh 10,000,000.00. Kwa ajili ya ukamilishaji darasa moja ambalo mpaka sasa Ukarabati unaendelea. Kanali Mwila ameelekeza ukamilishaji umalizike haraka na Amewapongeza wananchi katika kisiwa cha Buluza kwa kujenga Madarasa matano kwa Nguvu za wananchi na ofisi mbili ambazo bado zinajengwa na sasa zipo hatua ya lenta. 

Shule shikizi Lyegoba (mbinguni) Madarasa manne yaliyotolewa jumla ya Tsh 80,000,000.00 Ujenzi unaendelea hatua ya msingi (Hardcore) Kanali Mwila ameelekeza wasimamizi waongeze kasi kwani madarasa hayo yanatarajiwa kutumika mapema iwezekanavyo. 

Kanali Mwila amekagua Zahanati ya Kulazu na Shule ya msingi Kulazu iliyopo Kisiwa cha Kulazu Ambapo alibaini uhitaji wa watumishi wa zahanati na kupitia Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ameahidi kufanyia kazi ikiwa ni pamoja kupata Mtumishi katika zahanati hiyo.

Katika hatua nyingine Kanali Mwila amekagua Mradi wa maji Irugwa unaotekelezwa na Wakala wa Maji vijijini (RUWASA) wenye thamani ya Tsh. 584,000,000.00 Ambapo unatarajiwa kunufaisha watu 9000 Chanzo cha maji kimejengwa kijiji cha Sambi na kusambaza katika vituo vya kuchotea maji 18.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Kanali Mwila azungumza na wananchi wa Kata ya Irugwa katika Mkutano uliofanyika Shule ya Sekondari Irugwa na wananchi walipata nafasi ya kusema kero zao. 

Deus Magoma mkazi wa Kijiji cha Nabweko ameomba vituo vya maji kufika mpaka kitongoji cha Murutanga. Nae Datius Burchardi Kaimu Meneja wa RUWASA Ukerewe Ameeleza kuwa mradi ulilenga kukarabati chanzo, tanki, vituo 18 na mpaka sasa nyumba ya pampu choo na bomba zipo site na bado kulaza bomba. Ruwasa inaendelea kupitia vituo vyote na kuongeza vituo zaidi kwa kukabati vituo vilivyopo.

Bw. Daniel ametaka kuhakikishiwa kama ujenzi wa Kituo kipya cha afya au kuboresha zahanati iliyopo kijiji cha Sambi kuwa Kituo cha afya. 

akijibu hoja hiyo Mkurugenzi Mtendaji Bw. Emmanuel Sherembi amesema Irugwa inaundwa na sambi na nabweko kwanini tuvutane na vyote vinaletwa kwa ajili ya Irugwa. Fedha hii ya tozo za mawasiliano ineletwa kwajili ya ujenzi wa Kituo cha afya Irugwa kipya nasio upanuzi wa zahanati. 

 “awamu ya kwanza tumepokea Milioni 250 na tunatarajia kupokea fedha zaidi katika awamu ya pili”. Aliongeza Sherembi.


Filemoni Ladslaus mkazi wa kijiji cha Nabweko Amshukuru Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji kufika Irugwa kwa Mara ya kwanza na kujionea shughuli za Maendeleo katika kisiwa hiki. Ombi lake ni kuongezewa Bweni kwani wanafunzi wamefaulu wengi hivyo kuna uhitaji wa Bweni na ameomba Shule hii iwe na Kidato cha tano na sita.

Akijibu hoja hiyo Kanali Mwila amesema Kuanzishwa kwa Kidato cha tano na sita ni jambo zuri na muhimu hivyo taratibu zifuatwe kupitia Idara husika Na Suala la Bweni ni muhimu naomba muanzishe mchakato Wake.

Akitoa msimamo wa Serikali kuhusu wapi Kituo kipya cha Afya kitajengwa Irugwa Kanali Mwila amesema Kituo hiko kitajengwa katika kijiji cha Nabweko. “Ujenzi huu umelenga kuhudumia wananchi wa Irugwa na sio sambi pekee au nabweko pekee hivyo tuache mivutano tuijenge irugwa”. Alisema Kanali Mwila.

Irugwa imenufaika na hela za Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo na Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi y uviko19 katika Shule ya Sekondari Irugwa Madarasa sita tsh 120,000,000.00 na Shule shikizi ya Lyegoba  Madarasa manne Tsh 80,000,000.00 kwa Wilaya sasa tutaletewa Bilioni 3.5 kuboresha hospital ya Wilaya Nansio kuwa hospital ya Rufaa ya Mkoa. 

Madarasa yanayojengwa yatakua ni yakisasa vikiwa na umeme, vigae na miundombinu yote ya Muhimu kikubwa wananchi tuendelee kuchangia nguvu ili kubakisha Fedha zitakazotumika kutatua changamoto mbalimbali zilizopo katika Shule kama vile choo. 

Mhe. Joseph Sabato Msita Diwani kata ya Irugwa amshukuru sana Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji na kamati ya Ulinzi na wataalamu waliofika Irugwa kuangalia utekelezaji wa Miradi yote kisiwani hapo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.