• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

BARAZA LA MADIWANI LA AZIMIA KUILETEA UKEREWE MAENDELEO

Posted on: June 12th, 2019

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe limefanya vikao vyake vya kisheria ambapo limeketi kuanzia tarehe 11-12 juni. Baraza la Madiwani la Halmashauri linaloongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri na Diwani wa kata ya Kagunguli Mhe. George Machera Nyamaha na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri na Diwani wa Kata ya Bukindo Mhe. Gabriel Gregory Kalala pamoja na Katibu wa Baraza la madiwani na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ukerewe Bi. Ester A. Chaula. Wageni waliohudhuria baraza hilo ni pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Cornel Lucas B. Magembe na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Ukerewe ndugu Ally Mambile.

Baraza la Madiwani katika siku ya kwanza ya vikao vyake limejadili taarifa mbalimbali za maendeleo zinazotekelezwa katika kata. Kata zilizowasilisha taarifa zake na kuwasilishwa katika kikao ni pamoja na kata ya Nduruma, kata ya Namilembe, kata ya Murutunguru, kata ya Muriti, kata ya Namagondo na Kata ya Ilangala.

Baraza lilipata fursa ya kupata elimu juu ya CHF iliyoboreshwa na Mratibu wa CHF Mkoa wa Mwanza Bwana Kizito Wambura. Ameeleza kuwa wilaya ya Ukerewe ni moja kati ya Halmashauri 3 zenye vifaa vya kusajilia walengwa wa mfuko wa Bima ya CHF iliyoboreshwa katika mkoa wa Mwanza. Na mpaka sasa kaya 309 ambazo zinawanufaika 1715 zimesajiliwa kwa kupata huduma hiyo. Amewaomba madiwani kusaidia kuwaelewesha wananchi kuwa kuna umuhimu wa kujiandikisha kwani watanufaika kupata matibabu kuanzia zahanati mpaka hospitali za Rufaa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Mhe. George Nyamaha ameongoza baraza kujielekeza kujadili shughuli mbalimbali za maendeleo zilizotekelezwa katika robo ya tatu katika sekta mbalimbali kama ardhi upimaji shirikishi katika maeneo mbalimbali, ujenzi wa madarasa katika shule mbalimbali yamejengwa, afya vituo vinaendelea kuboreshwa.Baraza limeelekeza fedha zilizotolewa na serikali ikiwemo P4R zitumike kama ilivyoelekezwa na kufanya vizuri zaidi.

Aidha katika hatua nyingine Baraza la Madiwani kupitia mwenyekiti wa kamati ya Elimu Afya na Maji na diwani wa kata ya Kakerege Mhe. Sospeter Mgaya pamoja na makatibu wa vyama vya CCM na CHADEMA wamehoji kupewa sababu kwa nini maji katika vijiji vyenye miradi ya maji kutokutoka. Nae Kaimu Mhandisi wa Maji Wilaya Injinia Dartius Buchard ameeleza sababu hizo ni pamoja na kukatiwa maji kutokana na bili ya Umeme, shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji na baadhi ya mabomba kuharibika. Madiwani wameagiza kuwa ufuatiliaji ufanyike kwa ukaribu kuhakikisha changamoto hizo zinafanyiwa kazi.

Baraza la madiwani limepitisha na kuridhia wajumbe 9 watakao shughulika na baraza la kata la ardhi, ambapo kata za Kagunguli na Namilembe limepata wajumbe hao ambao watakuwa na kazi katika kutatua migogoro ya ardhi katika ngazi ya kata.

Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Cornel Magembe amewataka madiwani kusimamia Halmashauri ipasavyo katika kutekeleza majukumu yake. Ameomba baraza wakati mwingine wapate wajumbe katika mabaraza ya kata ya ardhi. Amepongeza madiwani kwani maendeleo yanayofanyika katika wilaya ya Ukerewe. Amewataka watumishi wa Halmashauri kujitambua na kutekeleza bila kusukumwa na madiwani.

Magembe ameagiza Idara ya Ujenzi kujielekeza kutumia milioni 12.5 ambazo zililetwa na serikali na P4R katika elimu msingi kujenga na kukamilisha jingo zaidi ya moja na maelekezo haya yameridhiwa na madiwani wote kuwa liwe ndio azimio la baraza.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ukerewe Bi. Ester A. Chaula amepokea maelekezo ya baraza na ametoa wito kwa madiwani kuendelea kushirikiana na menejimenti ilikufanikisha adhima kuu ya baraza na menejimenti ya kuwaletea wananchi maendeleo.

 “Lengo kuu la chombo hiki ni kufika mbali na kuiletea wilaya ya Ukerewe maendeleo na wilaya hii tukifanikiwa vizuri  wilaya yetu inauwezo wa kukusanya fedha na mapato mengi na kufikia nafasi ya tatu katika mkoa wa Mwanza” alisema Nyamaha akifunga mkutano wa Baraza la madiwani.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • UKEREWE YAANZA RASMI UTEKELEZAJI WA MRADI WA BOOST

    July 25, 2025
  • WATUMISHI IDARA YA AFYA WAASWA KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA MAADILI

    July 23, 2025
  • MKURUGENZI MBUA ASISITIZA MATUMIZI BORA YA MIFUMO YA SERIKALI

    July 22, 2025
  • WALIMU WAELEWESHWA DHANA YA UTHIBITI UBORA WA SHULE

    July 22, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.