• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

Chang’ah apiga marufuku uvuvi haramu na waliowapa mimba wanafunzi kukiona cha mtema kuni.

Posted on: July 20th, 2017

Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Estominh F. Chang’ah amepiga marufuku hiyo katika mkutano wa hadhara alipo kuwa akiongea na wananchi wa Nansio mkutano uliofanyika eneo la stendi ya zamani, mkutano ulimhusisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ndugu Frank S. Bahati na Mwenyekiti wa Halmashauri George M. Nyamaha.

Chang’ah katika hotuba yake mbali na kuzungumzia masuala ya ulinzi na usalama ambapo aliweka bayana kuwa kuna uwepo wa wageni wasio fahamika na kutokuwepo katika daftari la wakazi. Hivyo ataanza ukaguzi na amewaagiza maafisa tarafa, watendaji wa kata na kijiji kuhakikisha wageni wote majina na taarifa zao zinafahamika.

Chang’ah alibainisha mambo makuu mawili ambayo atayashughulikia ambayo ni mimba kwa wanafunzi na uvuvi haramu. Katika msako uliopita ilibainika kuna wanafunzi zaidi ya 100 walipata ujauzito, ijapokuwa tatizo kesi hizo za mimba zinakosa ushahidi kwani wazazi wanapoteza ushahidi kwa kushirikiana na watuhumiwa. Hivyo Mkuu wa Wilaya kwa kushirikiana na vyombo vya dola na Mkurugenzi mtendaji watahakikisha watuhumiwa wote  wanachukuliwa hatua za kisheria.

Ametoa rai kwa wavuvi wanafanya shughuli ya uvuvi katika ziwa victoria hasa upande wa Ukerewe kuachana na kujihusisha na matumizi ya zana haramu za uvuvi kwani unaharibu mazalia ya samaki ziwani hivyo serikali hivi karibuni itafanya msako mkubwa ili kutokomeza tabia hiyo. “Wote wanaojihusisha na uvuvi wa kutumia zana haramu za uvuvi kukiona cha mtema kuni” alisema Chang’ah.

Chang’ah ametaka utekezaji wa nyavu(zana za uvuvi) zitakazo kamatwa lazima wahusika wachukuliwe hatua za kisheria. “ukitaka kuishi kwa amani na raha katika serikali ya awamu ya tano fuata sheria, kanuni na taratibu za nchi” Chang’ah.

Chang’ah amewataka wananchi hususani vijana kuachana na tabia ya ukaaji vijiweni badala yake wajishughulishe kwa kufanya kazi ili kuweza kujipatia kipato kwani imeonekana wazee na wamama ndio wanajishughulisha katika maeneo mengi ya wilaya wakati vijana wanacheza “pool table”. Amekemea tabia hiyo na kuwataka kufanya kazi mbalimbali kama biashara na kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia fursa ya kuzungukwa na ziwa.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ukerewe Frank Bahati amekanusha dhana iliyojengeka miongoni mwa watu kuwa Ukerewe ni masikini hivyo ametoa rai wananchi kutoa ushirikiano kwa kulipa ushuru ila kuinua mapato na amesema mfumo wa ukusanyaji mapato utaimarika ili kudhibiti maeneo yote yenye mianya ya upotevu wa mapato.

Bahati alisema halmashauri imebuni miradi ya uvuvi endelevu kwani soko kubwa la samaki na dagaa litajengwa katika eneo ka Kamasi ambapo hekari 14 tayari zimepatikana kwaajili ya ujenzi huo na soko hilo litatoa fursa kwa wafanyabiashara kwenda kununua samaki hivyo kumuongezea mvuvi tija. Pia itaenda sambamba kabisa na uvuvi wa kisasa zaidi yani uvuvi wa kitalu ambapo mpaka sasa mchakato upo wizarani tayari kwa taratibu zingine.

Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. George Nyamaha ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano pamoja na baraza la madiwani katika kusimamia shughuli mbalimbali za maendeleo katika Nyanja zote na alibainisha changamoto ya iliyopo katika mabucha yaliyopo sokoni Nansio na kuwaondoa hofu wafanyabiashara hao kuwa ni ya serikali ni njema na kwa sasa ramani mpya ya vibanda vya soko kuu la Nansio imekamilika.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.