• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

DC NGUBIAGAI AKABIDHIWA KIZIMBA CHA KUZUIA WANYAMA HATARISHI ZIWANI

Posted on: November 25th, 2025

Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Cde. Christopher Ngubiagai amekabidhiwa kizimba maalum cha kujikinga na wanyama hatarishi wa ziwani ikijumuisha mamba na viboko mradi unaotekelezwa na taasisi ya utafiti wa wanyamapori "Tanzania Wildlife Research  Institute" (TAWIRI) ikiwa ni sehemu ya juhudi za serikali kuimarisha usalama wa wananchi wanaotumia fukwe kwa ajili ya shughuli mbalimbali wilayani Ukerewe.

Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika katika mtaa wa Namagubo B kata ya Nansio kilipo kizimba hicho Mkuu wa Wilaya amewataka wananchi kukitunza na kukilinda kizimba hicho.

"... ni vema kukilinda kizimba hiki kama mali yetu wenyewe, tukitumie kwa usahihi, tusikiharibu tuendelee kuwa mabalozi wa usalama katika vijiji vyote vinavyopakana na ziwa..." .

Ameongeza kuwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inagusa maisha ya wananchi kwa kuhakikisha usalama wa wananchi na uendelevu wa  raslimali za asili hasa kwa familia zinazoishi kandokando ya ziwa kwa kuleta vizimba hivi madhubuti.

Akitoa maelekezo kuhusu kizimba hicho Mwakilishi kutoka TAWIRI Anselm Munga amesema kizimba hicho ni sehemu salama kutumiwa kwa matumizi ya kawaida kama kufua nguo,  kuchota maji kwa usalama bila kubuguziwa na wanyama hatarishi kama mamba na viboko.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya ukerewe ndugu Vincent Mbua amewasihi wananchi kufanyia shughuli zao ndani ya kizimba hicho ili kupunguza na kudhibiti ajali zinazotokea kati ya binadamu na wanyama hatarishi.

Nae afisa wanyamapori wilaya ya ukerewe ndugu Zebedayo Timotheo amewasisitiza wananchi kuendelea kutumia kizimba hicho kwa umakini zaidi ili kiweze kudumu kwa muda mrefu.

Desdelia Dastan mkazi wa Namagubo B anaishukuru serikali kwa kuwajali na kuwakumbuka wananchi wao huku akisema wataendelea kutoa elimu kwa wananchi wengine juu ya matumizi ya kizimba hicho. Akihitimisha hafla hiyo Cde. Ngubiagai amewataka wananchi wa Ukerewe kuimarisha umoja na mshikamano na kulinda amani ambayo ni tunu ya taifa letu.

Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JKT- UKEREWE January 22, 2026
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA MILIONI 9O6.9

    January 19, 2026
  • MFUMO WA SIS KUONGEZA UFANISI SHULENI

    January 14, 2026
  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.