• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

DC NGUBIAGAI AKABIDHIWA MELI YA MV BUTIAMA KUANZA KAZI RASMI

Posted on: September 20th, 2025

 Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Cde, Christopher Ngubiagai amekabidhiwa meli ya MV Butiama tayari kuanza kazi baada ya kusitisha safari zake kwa ajili ya matengenezo kwa  takriban miezi 9 .

Akizungumza wakati akikabidhi meli hiyo kwa Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya TASHICO Anselm Namala amesema meli hiyo ilipata changamoto ya mizania ya meli ,serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kujali usalama wa wananchi wake ilibidi kusitisha huduma za meli hiyo ili ifanyiwe marekebisho .

" Meli hii ilifanyiwa majaribio siku kadhaa kabla ya kuruhusiwa kuanza safari zake, nawahakikishia imekuja ikiwa bora kwa viwango vilivyohakikiwa na wataalam wetu.Ratiba ni ile ile ikitokea Mwanza asubuhi saa 3 kwenda Ukerewe na kurudi saa 8 mchana."

Cde, Ngubiagai amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha sekta ya usafiri na usafirishaji kwa kuruhusu meli ya MV Butiama kuanza kutoa huduma kwani ni fursa ya kukuza shughuli mbalimbali za kiuchumi na ni ishara ya dhamira njema kwa serikali ya awamu ya sita kwamba hakuna mwananchi atakaebaki nyuma katika masuala ya maendeleo.

"..Wana Ukerewe tunajukumu la kuitunza meli hii ,tuvae umiliki kila mmoja awe mlinzi wa mali yetu.."

Nae mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Wilaya ya Ukerewe Mhe.Ally Khamis amesema ujio wa meli hiyo na vivuko vingine kama MV Bukondo, MV Ukerewe ni utekelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi katika maboresho ya sekta ya usafiri na kusisitiza kuwa serikali ipo kazini.

Daniel Majura mkazi wa Nansio anapongeza serikali ya awamu ya sita kwa kuona umuhimu wa kuboresha sekta ya usafiri kwa kuendelea kuongeza vivuko na kufanya maeneo mengi kufikika kwa urahisi.

Beatrice Bundala ni mkazi wa Kirumba Mwanza ni mfanyabiashara wa dagaa anashukuru serikali kufufua meli ya Butiama kwani sasa ana uhakika wa kuvuka asubuhi kuja Ukerewe na baadae kuvuka mchana akiwa na mzigo tayari kuingiza sokoni.

 Cde, Ngubiagai amehitimisha hafla hiyo kwa kuwataka wananchi wa Ukerewe kujitokeza kwa wingi katika kampeni za uchaguzi zinazoendelea kusikiliza hoja za wagombea ili ifikakapo Oktoba 29 ,2025 wawachague viongozi wanaowataka .

















Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI 2025 September 03, 2025
  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI AKABIDHIWA MELI YA MV BUTIAMA KUANZA KAZI RASMI

    September 20, 2025
  • JAMII TUNAWAJIBIKA KULINDA AMANI YETU - DC NGUBIAGAI

    September 19, 2025
  • WAJAWAZITO WASHAURIWA KUANZA KLINIKI MAPEMA

    September 18, 2025
  • MAFUNZO YA KANUNI NA MIONGOZO UENDESHAJI ZOEZI LA UTOAJI MIKOPO YA 10% YAZINDULIWA RASMI

    September 12, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.