• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

DC NGUBIAGAI AWAASA VIJANA KULINDA AMANI

Posted on: December 1st, 2025



"... amani siyo maneno bali ni vitendo, kila kijana awe muumini wa amani tunaweka michezo hii ili tuwe pamoja tufurahi na kushikamana kwa ajili ya Ukerewe na nchi yetu kiujumla..." Cde. Christopher Ngubiagai.

Ameyasema hayo alipohudhuria bonanza la Ukerewe one family lililowakutanisha Maafisa usafirishaji dhidi ya Machinga kwa mchezo wa soka katika uwanja wa Getrude Mongera Nansio huku Maafisa usafirishaji wakiibuka na ushindi wa bao Moja kwa sifuri.

Aidha Mhe.Ngubiagai amewataka vijana kushikamana katika nyanja zote huku akiwaahaidi kuwa serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan iko tayari kuwasikiliza vijana na kuipongeza serikali kuona umuhimu wa masuala ya vijana na kuanzisha wizara ya vijana hivyo wawe tayari kutoa mawazo yenye tija ili kuijenga Tanzania iliyo bora.

Nae Mbunge wa viti maalum kundi la vyuo vikuu Dr. Regina Malima amewataka vijana kujiepusha na maudhui yasiyofaa katika mitandao ya kijamii yanayoleta uchochezi wa vurugu huku akiwasihi vijana hao kutumia mitandao hiyo kwa faida kwa kujifunza vitu vipya na kutengeneza chaneli za biashara .

Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ukerewe ambae pia ni afisa michezo Ndugu Yehoshefati Kalulu Foda amewapongeza vijana hao kwa mchezo mzuri na wa kiungwana waliouonyesha na akiwaomba vijana kuwa chachu ya kuinua michezo katika wilaya ya Ukerewe.

Juma Hamis Tambwe ni nahodha wa timu ya maafisa usafirishaji yeye anaipongeza serikali kwa kuendelea kuwashika mkono vijana kwa kutoa fursa za mikopo ya 10% na kuahidi kuwa wataendelea kujituma kwa manufaa yao na taifa .

P. Man ni msanii wa kizazi kipya kutoka Nansio amepongeza uongozi wa Wilaya kwa kuanzisha Bonanza hilo huku akikiri kuwa ni sehemu ambayo wasanii wamepata mahali pa kuonyesha vipaji na kutangaza kazi zao.

Mkuu huyo wa Wilaya amehitimisha kwa kutoa zawadi ya Mbuzi mwenye thamani ya shilingi laki moja kwa mshindi wa kwanza mchezo wa soka huku mshindi wa pili akijinyakulia shilingi elfu 50 na kutangaza kuwepo kwa bonanza kubwa litakalofanyika Desemba 9, 2025 kuanzia asubuhi likuhusisha michezo mbalimbali.


















Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • UADILIFU NA UWAJIBIKAJI KWA WALIMU NI NGUZO YA MAFANIKIO

    December 03, 2025
  • DC NGUBIAGAI AWAASA VIJANA KULINDA AMANI

    December 01, 2025
  • AGENDA YA LISHE IWE YA KUDUMU

    December 01, 2025
  • WATOA HUDUMA ZA CHANJO 66 WAPATIWA MAFUNZO KUIMARISHA HUDUMA HIZO

    November 28, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.