• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

DC NGUBIAGAI AWAHIMIZA WANAUKEREWE KULINDA TAMADUNI ZAO

Posted on: January 18th, 2026

"... utandawazi na teknolojia ni tishio kwa utamaduni tusipokuwa makini, tuweni walinzi wa urithi wa tamaduni zetu, kwa ajili ya vizazi vijavyo, kama serikali tutaangalia uwezekano wa kuanzisha eneo la makumbusho kutunza maandiko ya waandishi wa fasihi kutoka hapa Ukerewe..."

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Cde, Christopher Ngubiagai alipokuwa akifunga simpozia ya kujadili namna ya kuhifadhi na Kutafiti Lugha, Fasihi na Tamaduni za Tanzania iliyoandaliwa na Chuo cha Napoli L' Orientale (UNIOR) Italia,Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT), Shirika la utafiti (ISMEO) na Shirika la Kuboresha Mienendo na Desturi kwa Ustawi (KUMIDEU) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Ukerewe.

Akiwasilisha mada ya utamaduni wa Kikerewe Mwenyekiti wa shirika la KUMIDEU Mzee Makubi Makubi amesema Ukerewe ni jamii iliyouishi ushirikiano katika nyanja zote za kijamii utamaduni ambao hadi hivi sasa unafanyika hasa katika masuala ya misiba na sherehe huku akitaja uwepo wa matambiko, ngoma za asili na utawala wa Kichifu kuwa nguzo imara zilizowaweka pamoja Wanaukerewe.

Roberto Gaudioso muadhiri kutoka chuo cha  UNIOR Italia ameonyesha jinsi ambavyo fasihi iliyoandikwa na Wakerewe ilivyoimara huku akimtaja Prof. Euphrase Kezilahabi kuwa miongoni mwa wandishi wakubwa wa fasihi na kuwasihi Wanaukerewe kuendelea kuzienzi kazi zake na kuzirithisha kwa vizazi vingine.

Suzana Mgaywa ni mdau wa utamaduni Ukerewe ameiomba serikali kuwa mstari wa mbele kutangaza vivutio vya utalii katika wilaya ya Ukerewe akitaja eneo la Handebezyo lililopo Halwego na fukwe mbalimbali zilizopo Ukerewe ambavyo havipatikani kwingine zaidi ya Ukerewe.

Mbali na masuala ya kutunza utalii Mhe. Ngubiagai amewataka Wanaukerewe kutunza mazingira hasa vyanzo vya maji na kupanda miti ili kuendelea kuiweka  Ukerewe salama sambamba na kuwavutia watalii na wadau wa maendeleo kuja kuwekeza kwa manufaa ya wananchi na serikali kwa ujumla.

Simpozia hiyo imetamatishwa na uwasilishwaji wa muziki wa Kikerewe kutoka Dunga Ngoma Group na Utandawazi Theatre Group (Matwi ga chalo) katika uwanja wa Getrude Mongella.

Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JKT- UKEREWE January 22, 2026
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA MILIONI 9O6.9

    January 19, 2026
  • MFUMO WA SIS KUONGEZA UFANISI SHULENI

    January 14, 2026
  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.