• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

DC UKEREWE APONGEZA WADAU KWA UJENZI WA SHULE YA WASICHANA

Posted on: August 8th, 2017

Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Estominh F. Chang’ah amefurahishwa na hatua nzuri ya ujenzi wa shule ya bweni ya wasichana inayojengwa kwa msaada wa marafiki kutoka marekani kupitia kanisa la Africa Inland Church (AIC), amesema hayo alipokwenda kutembelea na kujionea ujenzi wa shule hiyo yenye dhumuni chanya la kusaidia watoto wakike kupata elimu.


Wazo la ujenzi wa shule ya sekondari ya wasichana lilikuja kutoka kwa  mama wa kimarekani aliyekuja Ukerewe kufanya research ya PhD mwaka jana 2016 na katika kipindi hiko alibaini changamoto ya watoto wa kike wanaoishi mbali na shule ambapo wanakutana na vishawishi na wengine kuingia katika maadili maovu na kupata mimba za utotoni. Hivyo kwa kushirikiana na kanisa la AIC Dayosisi ya Mara na Ukerewe aliweza kuwasiliana na marafiki waishio marekani ikiwemo Hunter Parker na kupata hela zilizowezesha kuanza kwa ujenzi wa shule hiyo kubwa nay a kisasa ya wasichana itakayoitwa Tumaini Jipya Girls Secondary School.

James Mnubi ambaye ni msimamizi wa ujenzi wa shule hiyo amesema ujenzi utakua na awamu mbili ambapo katika awamu ya kwanza ujenzi utagharimu shilingi Bilioni 4, na miundombinu itakayojengwa ni Nyumba za walimu 8,madarasa 8, mabweni 4, vyoo vya walimu na wanafunzi. Ambapo mpaka sasa miundombinu iliyokamilika ni madarasa mawili, bweni na vyoo matundu saba na moja kwa wenye mahitaji maalumu, na jingo la utawala linatarajiwa kuanza na kukamilika kabla ya ufunguzi wa shule hiyo mkombozi hapo January 2018. Awamu ya pili itahusisha ujenzi wa madarasa kwa ajili ya kidato cha tano na sita.

 Chang’ah amepongeza wadau hao wa elimu kwa hatua nzuri ya ujenzi wa shule hiyo itakayo mkomboa mtoto wa kike katika mazingira magumu ya masomo na kuwaepushia vishawishi na kuondokana na tatizo la mimba za utotoni. “Nimefurahishwa sana na hatua hii kwani sasa naamini elimu wilayani ukerewe itazidi kuinuka hasa kwa wasichana na tutatoa ushirikiano kuhakikisha lengo la elimu bora kwa wasichana linatimia” alisema Chang’ah.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.