• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

FFS WAKABIDHI MADAWATI 126 UKEREWE

Posted on: February 22nd, 2021

Shirika la Huduma kwa Wakulima (FFS) chini ya ufadhili wa Rotary Club wamekabidhi madawati 126 yenye thamani ya Tsh 6,250,000/- kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe, hafla iliyofanyika makao makuu ya Halmashauri na kushuhudiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Cornel Magembe.

Mwenyekiti wa Bodi ya FFS Bw. Makubi amepongeza hatua ambayo Asasi hii kwa kuwa mfano wa kuigwa na Asasi zingine ndani na nje ya Wilaya ya Ukerewe. 


Mratibu wa FFS Bw. Reuben Richard ameeleza Mradi wa kutengeneza madawati 126 umeanza mwezi oktoba 2020 na kila dawati limegharimu Tsh. 50,000/- kazi iliyofanyika katika Shule ya ufundi Bukongo. 

“Madawati haya yatasaidia kupunguza uhaba mkubwa wa madawati uliopo mashuleni” Alisema Richard. Aidha Matarajio yetu ni kutenengeneza madawati zaidi ya 200 na mpaka sasa baada ya kutoa dawati 126 tumebakiza dawati 100 ili kufikia lengo kwa mwaka huu. Aliongezea Richard.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Bi. Ester Chaula ameshukuru Shirika la FFS na Rotary Club kwa kuunga mkono sekta ya elimu ambayo ndio msingi kwa elimu ya mtoto. 

Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Joshua Manumbu amepongeza mashirika hayo kwa kuendelea na wadau wazuri wa Maendeleo katika Wilaya ya Ukerewe ambapo Rotary Club wamefanya pia katika Sekta ya kilimo na maji pia.


Mkuu wa Wilaya Mhe. Cornel Magembe ameshukuru wadau na Asasi hizo kwa kushirikiana na Serikali katika kutoa huduma. Amewasihi Asasi zingine za kiraia kujitokeza ili kupunguza upungufu huo.

“Kuna upungufu wa madawati zaidi ya 4000 kwa Shule za Msingi na Sekondari bado tunaendelea kuhitaji wadau kutuunga mkono” alisema Magembe.


Aidha amewaomba wananchi ambao ni wazawa wa Ukerewe kuja na kuchangia miundombinu hasa ya Elimu na Afya. “nawaalika wote walioko maeneo mbalimbali mikoani na duniani kuja tushirikiane katika shughuli za Maendeleo”. Aliongeza Magembe. 

Salila mfungo Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Kalendelo Amesema Shule hiyo kwa kushirikiana na wananchi imejenga darasa 3 na yameezekwa. Tunashukuru kwa madawati haya yatapunguza upungufu wa dawati. Shule ya Msingi Kalendelo imepatiwa madawati 40, 

Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JKT- UKEREWE January 22, 2026
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA MILIONI 9O6.9

    January 19, 2026
  • MFUMO WA SIS KUONGEZA UFANISI SHULENI

    January 14, 2026
  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.