• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

HISTORIA MPYA YAANDIKWA SIZU, MONGELLA AWA MKUU WA MKOA WA KWANZA KUFIKA

Posted on: February 11th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella ameanza ziara ya kikazi katika Wilaya ya Ukerewe na ametembelea Zahanati kijiji cha Sizu kata ya kagunguli na kukagua zahanati hiyo pamoja na namna huduma zinavyotolewa. Ikiwa ni mara yake ya kwanza kama Mkuu wa Mkoa kuwahi kufika katika kisiwa hiko tokea Uhuru. Ameeleza adhma yake kupitia ziara hiyo kuhakikisha anatembelea visiwa vyote vinavyounganisha kisiwa cha Ukerewe.

Elizabeth John Amos Tabibu Msaidizi wa Zahanati ameeleza kuwa imeweka mikakati ya kupunguza vifo vya wakinamama na watoto, kutoa Elimu na kutumia dawa za kuongeza Damu na kuhudhuria cliniki mapema.“Ufinyu majengo ya kutolea Huduma za Afya kwani Mpaka sasa jengo lilopo ni moja tuu, Uhaba wa watumishi ambapo kituo kinawatumishi wawili.” Alisema Elizabeth.

 Mongella ameahidi kishughulikia changamoto hiyo pamoja na kupata jengo la kujifungulia Katika zahanati hiyo. Na amewapongeza watoa huduma katika zahanati hiyo kwa kuendelea kuwahudumia wananchi.

Katika shule ya Msingi Sizu Mkuu wa Mkoa amechangia kiasi cha Tsh 100,000, Tsh 50,000/- kutoka kwa afisa Elimu Mkoa, na Mkuu wa Wilaya Mhe Cornel Magembe ameahidi mifuko 10 ya saruji.


Mongella ametembelea kisiwa cha Kweru mto ambapo amekagua shule shikizi ambayo imejenga madarasa manne pamoja na ofisi ya walimu mradi uliogharimu Tsh 33,000,000/- ambapo inahusisha mchango wa Mkurugenzi, Mchango wa wananchi pamoja, NMB pamoja na mifuko 193 ya saruji fedha za Mfuko wa jimbo, katika kisiwa hiko Mongella apepongeza wanakweru mto kwa jitihada hizo na ameahidi kuwa atafuatilia madarasa mawili yaliyosalia pamoja na ujenzi wa Choo ili shule hiyo ipatiwe usajili kamili.

Mongella amefurahishwa na hali ya kujitoa ya wananchi wa kisiwa hiko katika kuchangia maendeleo yao kwa kujenga shule hiyo, hivyo ametoa ahadi ya kuchangia mabati 100 ili wakamilishe majengo yaliyosalia.

Awali mwenyekiti wa Halmashauri Mhe George Nyamaha amemweleza adhma ya wananchi wa kisiwa hiko kuwa ni kuboresha Elimu na wapo tayari kukamilisha ujenzi kwa mifuko iliyotolewa na mbunge ili kupatiwa usajili.
Akiwa Katika kisiwa cha Irugwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella amesema atafuatilia upatikanaji wa Meli ya kubeba abiria na anaamini Mhe. Dkt John Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni msikivu katika mahitaji ya wananchi. Ameeleza hayo kufuatia ombi la Mkuu wa Wilaya juu ya Adha kubwa ya usafiri wapatayo wanairugwa.
Mhe Joseph Mkundi Mbunge wa Ukerewe (CCM) amewapongeza wanairugwa kwa kutumia vema mifuko 200 ya saruji zilizotolewa na mfuko wa jimbo pamoja na miundombinu yote iliyotolewa na serikali ya awamu ya Tano.

“Pamekuwa na changamoto ya watu wengi kukosa namba za vitambulisho vya taifa, hivyo nawataka watumishi wa NIDA wilaya kutoka na kuwafuata watu na kuwapatia namba na ambao hawajaandikishwa kupatiwa huduma hivyo kufikia tarehe 14 februari.” Alisema Mongella.

Amewataka wananchi kuachana na uvuvi wa kutumia zana haramu kwani unaharibu mazalia ya samaki na hairusiwi kisheria hasa za nchi yetu ya Tanzania.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.