• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

KAMBI TEMBEZI YA MATIBABU BILA MALIPO YAZINDULIWA RASMI

Posted on: November 17th, 2025

Serikali kupitia divisheni ya afya wilayani Ukerewe kwa kushirikiana na Canada African Community Health Alliance (CACHA) imeendelea kuwathamini wananchi wake kwa kuanzisha kambi tembezi ya matibabu bila malipo itakayofanyika kwa vituo tisa kuanzia Novemba 17 hadi 27, 2025 kwa magonjwa yote ya ndani, magonjwa ya meno, macho, Saratani ya matiti na mlango wa kizazi, huduma za watoto na akina mama sambamba na huduma za upimaji.

Akizungumuza katika ufunguzi wa kambi hiyo uliofanyika katika kituo cha afya cha Igalla kilichopo kata ya Igalla Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Cde, Christopher Ngubiagai amewataka wananchi kuupokea mpango huo wa serikali ili kuleta ustawi wa jamii ya Ukerewe.

"... tunafahamu gharama za kupata matibabu ni kubwa sana hivyo serikali imeona ni vema kuwasogezea wananchi matibabu haya yanayo tolewa bila malipo ili tuweze kuwa na jamii yenye afya,umoja, amani, mshikamano na nguvu za kufanya kazi ili kuleta ustawi kwa wilaya yetu ya ukerewe ..." Cde Ngubiagai.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Dkt. Charles Mkombe ameipongeza serikali kwa mpango huo madhubuti wa kuwapelekea wananchi huduma huku akisema kutakuwa na ongezeko la siku saba za upasuaji katika hospitali ya Wilaya .

Nae daktari kiongozi wa kambi hiyo Bunhya Kayila amewasisitiza wananchi kuendelea kujitokeza katika vituo vyote vilivyoainishwa kwa ajili ya kupata matibabu hayo kwani timu ya madaktari ipo tayari kuwahudumia.

Maza Mlele ni mkazi wa kijiji cha Chankamba yeye amesifu jitihada za serikali kuwakumbuka  wananchi wanaoishi mbali na huduma za afya za kibingwa kwa huduma hizo zinazotolewa bila malipo huku akikiri kuwa ni mkombozi kwa wananchi.

Akihitimisha ufunguzi huo Mkuu wa Wilaya amewataka wananchi wa Ukerewe kudumisha amani na utulivu ili serikali iweze kuwa huru kuleta huduma bora na maendeleo katika jamii ya Ukerewe.


















Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JKT- UKEREWE January 22, 2026
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA MILIONI 9O6.9

    January 19, 2026
  • MFUMO WA SIS KUONGEZA UFANISI SHULENI

    January 14, 2026
  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.