• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

KAMWELWE AZINDUA KIVUKO CHA MV.UKARA II “HAPA KAZI TU’’

Posted on: October 19th, 2020

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na mawasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe amefanya uzinduzi wa kivuko cha MV.Ukara II “HAPA KAZI TU” kitakacho safirisha abiria kati ya Bugorola na kisiwa cha Ukara katika wilaya ya Ukerewe mkoani  Mwanza. Uzinduzi  huo uliofanyika leo tarehe 19/10/2020 katika kisiwa cha Ukara na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Adam Malima, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Cornel Magembe na viongozi mbalimbali wa chama,  Taasisi mbalimbali za Serikali  na Viongozi wa dini.

           Akizungumza kwenye uzinduzi huo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe ameagiza mtendaji mkuu TEMESA kurekebisha ratiba ya meli  hiyo na  kuhakikisha inatoka mapema Ukara ili watu wawahi meli za kwenda Mwanza kutoka Nansio ikiwemo MV Butiama. “ TEMESA ihakikishe ratiba irekebishwe na wanaukara wawekaribu na Mwanza” alisema Kamwelwe.

“Natoa ofa meli hii ibebe abiria katika safari zake kwa siku mbili bure bila mtu kutoa nauli ili kila mwanaukara kwa siku hizi mbili afurahie huduma na meli yetu hii mpya” aliongeza Kamwelwe.

Aidha Kamwelwe amewaagiza TASAC kuendelea kutoa mafunzo kwa wamiliki, waendeshaji na watendaji mbalimbali wa vivuko ikiwemo TEMESA kwa  kuzingatia taratibu na kanuni za uendeshaji wa vivuko  ili kupunguza ajali za majini.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella amshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi, na Mawasiliano, TEMESA na Songoro MARINE LTD kwa kujenga kivuko cha MV Ukara II “HAPA KAZI TU” ambacho kitapelekea kukua kwa uchumi wa wananchi wa Wilaya ya Ukerewe na watanzania kwa ujumla kwa kufanya usafiri na  usafirishaji wa mizigo na abiria.

Akisoma taarifa fupi ya kivuko cha MV Ukara II “HAPA KAZI TU”, Mtendaji Mkuu wa TEMESA Mhandisi Japhet Masele amesema kivuko hicho kina urefu wa mita 42 na upana wa mita 10 chenye uwezo wa kubeba uzito wa tani 100 ambao ni sawa na abiria 300 na gari ndogo 10. “MV Ukara II “HAPA KAZI TU” imegharimu kiasi cha shilingi Bilioni 4.2. Alisema Masele.

Aidha Mhandisi Masele amesema Kivuko cha MV Ukara II “HAPA KAZI TU” kimefungwa vifaa vya mawasiliano ikiwemo DIRA (Compass Direction) kwa ajili ya mawasiliano. Pia amesema MV Ukara II “ HAPA KAZI TU” kina chumba maalumu kwa ajili ya wagonjwa na kimefumgwa vifaa vya uokoaji ikiwemo maboya.

Mkuu wa Wilaya wa Ukerewe Mhe. Cornel Magembe ameishukuru Serikali ya awamu wa tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kwa kushirikiana na Wananchi wa Ukerewe baada ya ajali ya meli ya MV Nyerere iliyotokea Septemba 2018 na kuahidi kutengeneza kivuko kipya kwa ajili ya wananchi na leo Ukara imepokea kivuko cha MV Ukara II “HAPA KAZI TU”.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.