• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

KANDEGE APONGEZA WANANCHI KUJITOA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU UKEREWE.

Posted on: February 27th, 2020

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Josephat S. Kandege ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Vyumba vya madarasa manne na ofisi moja katika Shule ya Msingi Murunsuli.

Kandege amepongeza wananchi wa kata ya Ngoma kwa kuonyesha mshikamano na kujenga vyumba hivyo vya madarasa ikiwa na lengo la kukabiliana na upungufu wa Madarasa.

Mhe Cornel Magembe Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe ameeleza kuwa kwa kupitia nguvu za wananchi na uhamasishaji aliofanya zaidi ya vyumba vya madarasa 316 vinejengwa na vipo vilivyoanza kuezekwa na Halmashauri na vingine Bado.

Magembe ameomba wizara kuangalia na kuwezesha fedha ilikuweza kuenzeka maboma hayo. Amewapongeza wananchi wa Murunsuli kwa kujenga madara hayo na sasa yapo katika hatua ya kuweka madirisha na ukamilishaji.

“Hakika kuna vingi vya kujifunza kutoka ukerewe hongereni wananchi kwa ujenzi huu na wengine igeni mfano huu”. Alisema Kandege.

Gharama za Ujenzi wa Vyumba vinne vya madarasa na ofisi moja ya waalimu Halmashauri imetoa Tsh 13,054,000/-, michango ya wananchi Tsh 11,000,000/-, nguvu za wananchi 6,000,000/-.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Josephat S. Kandege amekagua shughuli za utendaji kazi wa vikundi vya kijamii ambavyo vimepatiwa mkopo na Halmashauri kupitia vikundi ambapo ni utekelezaji wa Sheria kuwa asilimia 10 ya pato la Halmashauri inatakiwa kukopeshwa wanawake vijana na watu wenye ulemavu.

Kandege ameelekeza Halmashauri kupitia Idara ya Maendeleo ya jamii kuongeza kiasi cha mkopo na kuwa kiwango cha chini kikundi kukopeshwa kiwe TSH 5,000,000/-.

Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo Secilia Oswago ameeleza Halmashauri inatekeleza sheria hiyo na vikundi alivyotembelea Naibu waziri vimewezeshwa kikundi cha Tumaini Jema kata ya Kagera kimekopeshwa TSH 5,000,000/- na chama cha watu wenye ualbino kimekopeshwa TSH 2,000,000/- na wote wanatarajiwa kurejesha baada ya mkopo ili kutoa nafasi kwa vikundi vingine kukopeshwa.

Bi. Ester A. Chaula Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ameeleza kuwa Halmashauri inaendelea kutoa mikopo hiyo na kwa mwaka huu wa fedha Halmashauri imeshatoa jumla ya TSH 103,950,000/- na Bado utoaji wa mikopo mingine utafanyika.

Kandege amepongeza vikundi hivyo kwa ubunifu walionao kwani bidhaa zao ziko katika ubora unaotakiwa.

Aidha Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Josephat S. Kandege ametembelea na kukagua majengo na utoaji Huduma katika kituo cha Afya Bwisya kilichopo kata ya Bwisya Tarafa ya Ukara.

Kandege ameridhishwa na Kituo cha Afya hiko ambapo amepongeza Serikali ya Wilaya ya Ukerewe kwa kutekeleza vema ujenzi huo ulio gharimu takribani Bilioni 1.2.

“Ukiita Kituo cha Afya unakua hutendi haki kinastahili kuitwa Hospitali ya Wilaya” alisema Kandege.

Mhe Cornel Magembe Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe ameeleza mahitaji yote yanayohitajika katika kituo hiko ilikufanya kuwa Hospitali ya Wilaya ikiwemo watumishi na baadhi ya vifaa yamesha wasilishwa Wizarani na nimatumaini kuwa yatafanyiwa kazi.

Kandege ameeleza kuwa Adhma ya Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dkt John Magufuli ni kuhakikisha Afya za wats za is zinaimarika hivyo ametangaza kuajiri madaktari 1000 ambapo ajira za madktari 750 zitakua TAMISEMI hivyo ameahidi ataleta madaktari wasiopungua watatu katika kituo hiko.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.