• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

KANGI AAGIZA KUKAMATWA NA KUCHUKULIWA HATUA WOTE WALIOHUJUMU MRADI WA MIL 317 UKEREWE

Posted on: January 23rd, 2018

Ziara ya Mhe. Kangi Lugola tarehe 23/01/2018 Wilayani Ukerewe Kutembelea na kukagua mradi wa ufugaji wa samaki kwenye mabwawa kwa kutumia nguvu ya umeme wa jua. Mradi huo utekelezaji wake umefanyika katika kata ya Namagondo. Ziara ilianza kwa Mhe. Naibu Waziri kufika ofisi ya Mkuu wa Wilaya na kupokelewa na viongozi wa Wilaya ambapo pia alipokea Taarifa ya Wilaya.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Lugola ameutaka uongozi wa Wilaya ya Ukerewe kushirikia katika kuhakikisha Mazingira yanatunzwa kama ilivyoelekezwa katika Ilani. Amewataka pawepo na jitihada za makusudi katika kuhakikisha Miti inapandwa kwa wingi, mitaro inayopitisha majitaka inaondolewa udongo kama ilivyoelekezwa na mazingira yanatunzwa kwa ustawi wa vizazi vijavyo na kuwepo kwa hali nzuri ya hewa.

Utekelezaji wa Mradi wa Ufugaji wa samaki kwenye mabwawa kwa kutumia nishati ya jua ulianza mwezi April 2015, ukihusisha wadau mbalimbali ambao ni kikundi cha Pambazuko, shirika lisilo la kiserikali la ECOVIC ambao ndio wasimamizi wa mradi, Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe, Taasisi ya Utafiti ya Uvuvi na shirika la Maendeleo la UNDP ambao ndio wafadhili wa Mradi kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Ofisi ya Mak,amu wa Rais. Mradi Huo umegharimu Milioni 240,600,000 tu alisema Jackson Ndobeji pesa ambayo iliwekwa kwenye akaunti ya ECOVIC kwaajili ya shughuli za usimamizi na utunzaji wa kumbukumbu zote za fedha na kukamilisha ujenzi wa mabwawa 24 ambapo siita (6) ya SATO na (18) mumi na Kambare ambapo eneo zima la mradi ni ekari 30.

Lengo la mradi ni kutoa elimu ya ufugaji wa samaki kwenye mabwawa kupitia nishati ya jua, kutunza mazingira, upatikanaji wa lishe bora na kuondokana na umasikini, alisema Ndobeji. Pia ameainisha madhumuni yao ambapo ni pamoja na kufungua kituo cha kuzalisha kituo cha kuzalisha chakula cha samaki na kusaidia wafugaji wadogo na kuongeza mazalia ya samaki na kuongeza wastani wa kipato. Shughuli zilizofanyika ni pamoja na kuandaa eneo la mradi, mafunzo kwa wanakikundi kutembelea Misungwi na Muleba, stoo ya kutunza zana za mradi, uchimbaji wa mabwawa na uwekaji wa miundombinu na vifaa vya maji, mashine ya kusaga imefungwa na imenunuliwa, mashine ya kusukuma maji, ununuzi wa matanki ya kuzalishia vifaranga, ujenzi choo boma limekamilika na kufunikwa,wigo eneo la kufugia kwa ajili ya usalama ufyekaji wa nyasi kuzuia mmomonyoko wa udongo. Alisema Ndobeji.

Baada ya Ukaguzi wa eneo la mradi Mhe Naibu Waziri Kangi Lugola aliainisha kuwa fedha hizo zilizotolewa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, na kwa kutambua kuwa nchi yetu imeanza kukumbwa na mabadiliko ya tabia ya nchi, na athari kwenye kilimo, hivyo katika nchi nzima zilichaguliwa Wilaya tatu (3) ambazo ni Chamwino, Bahi na Ukerewe ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais iliomba fedha kwa wafadhili. Mradi ulilenga kunufaisha vijiji kumi na kusaidia kilimo katika eneo hilo. Na yalitakiwa kujengwa mabwawa manne (4) ya kutotolea samaki kitu ambacho hakikufanyika na madala yake walinunua matanki manne.

Kangi alibainisha kuwa thamani halisi ya Mradi huo ni Milioni 317,400,000/= mabapo pesa hizo hazisadifu kilichofanyika badala yake inaonekana ni pesa chache ndizo zilizotumika hapo na mratibu wa mradi huo ndugu Jackson ndobeji kusema kuwa fedha zimeisha na hivyo walihitaji fedha zingine. Kangi amesikitishwa na kutokukamilika kwa mradi na amesema serikali ya Magufuli haijaribiwi bali ipo kutetea wanyonge na kupambana na mchwa wanaokula fedha za wananchi. Mratibu wa mradi alishindwa kusema ukweli juu ya thamani halisi ya mradi huo hivyo mradi kutokukamilika. “Haiwezekani mtu mmoja kusababisha madhara makubwa na kurudisha nyuma maendeleo ya wananchi.” alisema Kangi.

Baada ya kubaini ubadhilifu wa fedha hizo za mradi wa samaki Namagondo kutokuwepo na kushindwa kukamilika na kushindwa kutengeneza barabara ya km.4.5 kama ilivyoainishwa kwenye mkataba, Mhe. Kangi Lugola ameagiza kukamatwa kwa Mratibu wa ECOVIC Bwana Jackson Ndobeji na ameagiza TAKUKURU na vyombo vya dola kukamatwa wote waliopo kuanzia ofisi ya makamu wa rais na wote walioko shirika la UNDP walioshirika katika ubadhilifu huo na wafikishwe mahakamani.

 Kangi amemtaka Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kufuatilia kwa ukaribu miriadi yote inayotekelezwa ndani ya Wilaya hata kama mtu amejitolea thamani ya fedha zinazotumika zifahamike na pawepo uwazi na kushirikisha Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya. Kupitia ofisi ya Makamu wa Rais watakaa na kuona jinsi gani ya kufufua mradi huo na pesa kutokupotea bure.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.