• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI IONGEZEKE

Posted on: December 1st, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike Leo ameanza Ziara ya siku mbili kukagua miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika Wilaya ya ukerewe ambayo ni ujenzi wa madarsa katika tarafa za ukara na mumlambo lengo likiwa nikukagua Kituo cha Afya Bwisya ambayo itakua na hadhi ya Hospitali ya Wilaya na ujenzi wa madarasa  Fedha iliyotolewa na Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Uviko19.

Samike ametembelea Miradi kisiwa cha Ukara na amewataka amewataka wakuu wa Shule na kamati inayosimamia ujenzi kuhakikisha inasimamia kwa ukaribu utekelezaji wa miradi hiyo ili iweze kukamilika katika ubora unaotakiwa. 


Aidha Amelekeza kuwa Shule za Sekondari Bukiko, Nyamanga na Bwisya kupanda miti katika maeneo yao hii italeta mandhari nzuri ya Shule na utunzaji wa mazingira. 


Katika hatua nyingine Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike ameelekeza kasi iongezeke katika utekelezaji wa ujenzi wa madarasa na kuhakikisha ubora unazingatiwa na Miradi yote ikamilike kwa wakati. 


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ukerewe Bw. Emmanuel Sherembi ameeleza kuwa kwa changamoto za kisiwa cha Ukara nyingi zimetatuliwa na miradi inaendelea vema. 


Katika Tarafa ya Ukara ametembelea Shule za Sekondari Bwisya inayojenga madarasa 5, Nyamanga inayojenga madarasa 7, na Bukiko inayojenga madarasa 4 na Tarafa ya Mumlambo ametembelea Shule za Sekondari Bukindo inayojenga madarasa 8, Pius Msekwa inayojenga madarasa 5 na Tarafa ya Mumbuga amekagua Shule ya Sekondari ya Bukongo inayojenga madarasa 3 ambapo kila darasa Serikali ilitoa Tsh. 20,000,000.00.

Katika siku ya pili ya ziara yake Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike ameendelea na ziara ambapo amepata nafasi ya kuzungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe na ametembelea Miradi ya Maendeleo katika kisiwa Kikubwa cha Ukerewe. 


Samike akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe amewataka waendelee kufuata Sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa Umma. “ kila Mtumishi kwa nafasi yake anawajibu wa kutekeleza mambo yote ya msingi kwa kufuata sheria na miongozo ya utendaji kazi ili kutoa Huduma bora kwa wananchi” Alisema Samike. 

Aidha amemuelekeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kuhakikisha anasimamia kwa ukaribu ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri na kuwezesha Halmashauri kujiendesha katika shughuli za kila siku.


Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Bw. Emmanuel Sherembi ameahidi kuhakikisha mapato ya Halmashauri yanakusanywa kwa uaminifu na kuziba mianya ya upotevu wa mapato.


Katika hatua nyingine Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza amekagua Ujenzi wa Madarasa katika Shule za Sekondari Nakatunguru waliopatiwa Tsh. 60,000,000.00 kujenga madarasa matatu na sasa wapo hatua ya kupandisha kuta usawa wa madirisha, Shule ya Sekondari Bukanda iliyopewa Tsh. 100,000,000.00 kujenga madarasa matano na wapo hatua ya kukamilisha kupiga kenchi na Shule ya Sekondari Mumbuga iliyopewa Tsh. 120,000,000.00 kujenga madarasa 6 na mpaka sasa wapo hatua ya kupandisha kuta. 

“Ongezeni kasi ya ujenzi wa madarasa na yakamilike kwa wakati uliopangwa na Serikali” Alisisitiza Samike.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.