• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

KIMBUNGA CHALETA MAAFA UKARA

Posted on: October 20th, 2017

Wananchi wa kata ya Bukiko kijiji cha Bukiko wamepatwa na maafa ya kimbunga ambapo maafa yamekumba kaya za wananchi, maeneo ya taasisi za serikali kama nyumba ya waalimu, soko la kijiji, jengo la nyumba mali ya chama cha mapinduzi(CCM). Wananchi wa Bukiko walikumbwa taharuki ya kimbunga hiko mnamo saa kumi usiku wa kuamkia tarehe 19 oktoba na kuwaacha wakiwa katika sintofahamu ya hali ambayo haikutegemewa.

Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Mhe. Estomihn Chang’ah  amewapa pole wananchi wote wa Bukiko waliopatwa na janga la kimbunga hiko. Amewataka wananchi kuwa na umoja katika kipindi hiki cha tatizo hilo na kuhifadhiana na kusaidiana pale panapohitajika kwani tatizo halina hodi. Alisema Chang’ah.

Amewataka wananchi wazingatie ujenzi bora wa miundombinu ya nyumba za kuishi kwani nyumba zikiwa imara itapunguza maafa ya uharibifu kwani hazita shambuliwa na upepo huo mkali. “Tujenge nyumba zetu katika ubora kwa kuzingatia kanuni thabiti za ujenzi ili tusikumbwe na maafa ya namna hii kwani tukiwa na nyumba imara hazitaezuliwa”. Chang’ah.

Katika kuwafariji wahanga wa kimbunga hiko Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ndugu Frank Bahati amewapa pole wote waliukumbwa na matatizo hayo na kuwataka kuwa na ushirikiano. Alieleza kuwa mtaalamu wa ujenzi ameambatana nae ili kufanya tathimini ya madhara yaliyosababishwa na upepo huo mkali na kwa miundombinu ya taasisi za serikali iliyo athirika na upepo huo zitafanyiwa marekebisho ili ziendelee kutoa huduma kwa wananchi.

Maepongeza serikali ya kata na kijiji kwa kushirikiana kikamilifu na wahanga na kuhakikisha nyumba za taasisi za serikali kama nyumba ya waalimu iliyoezuliwa na kuwaacha walimu watatu kukosa makazi na kuwahifadhi na kuanza utaratibu wa kurekebisha makazi yao ili waendelee na kazi ya ufundishaji kwa wanafunzi.

Makamo mwenyekiti wa Halmashauri Greygor Kalala alitoa pole pia kwa wahanga hao na kuwataka waepukane na tabia ya kuhusisha majanga ya kimazingira na siasa. Amewataka kuimarisha umoja wao kama wakara na wakerewe na watanzania kiujumla kwani tatizo siku zote halina hodi.

Crispin Nswasa ambaye ni Mtendaji wa kata hiyo ameeleza kuwa kaya zaidi ya ishirini (20) zimepatwa na maafa hayo pamoja na uharibifu katika paa la soko la kijiji na mashine ya kikundi. Alieleza kuwa upepo huo mkali aina ya Msoke ulianzia ziwani na kuelekea katika eneo la makazi ya watu ambapo uliambatana na mvua. Upepo huo mkali ulikua na uwezo wa kubeba paa na kulitupa umbali wa zaidi ya nusu kilometa.

Mmoja wa waathirika wa maafa hayo ambaye nyumba yake iliezuliwa ameshukuru kwa dhati serikali ya Wilaya kwa kujali na kwenda kuwapa pole. “Tunafarijika sana tukiona uongozi unajali wananchi wake hasa sisi tuliokumbwa na maafa haya na kutuacha na magofu”. Alisema Mwananchi huyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • UKEREWE YAANZA RASMI UTEKELEZAJI WA MRADI WA BOOST

    July 25, 2025
  • WATUMISHI IDARA YA AFYA WAASWA KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA MAADILI

    July 23, 2025
  • MKURUGENZI MBUA ASISITIZA MATUMIZI BORA YA MIFUMO YA SERIKALI

    July 22, 2025
  • WALIMU WAELEWESHWA DHANA YA UTHIBITI UBORA WA SHULE

    July 22, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.