• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

UKEREWE YAANZA RASMI UTEKELEZAJI WA MRADI WA BOOST

Posted on: July 25th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kupitia idara ya elimu msingi imeanza utekelezaji wa mradi wa BOOST kwa kufanya kikao na wataalam wa kada mbalimbali wanaohusika pamoja na wasimamizi wa miradi katika maeneo husika ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha kuwa fedha zote zinatumika kwa kufuata maelekezo yaliyotolewa na kutoa matokeo chanya.

Akizungumza wakati wa kikao hicho elekezi kilichokuwa na lengo la kujenga uelewa wa pamoja kwa wahusika wote juu ya namna ya kutelekeza miradi hiyo kwa ufanisi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo ndugu Chinchibera Wanchoke ameanza kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu shilingi Bilioni 2.5 zije Ukerewe kwa ajili ya miradi ya elimu huku akieleza umuhimu kwa wananchi wa maeneo ya miradi kupata taarifa kwa usahihi ili washiriki kikamilifu kukamilisha miradi hiyo.

".. miradi hii ni ya wananchi ni lazima wajue kinachoendelea kwa usahihi ili tupate wepesi katika utekelezaj wake, tutembee katika uongozi wa kuacha alama.." amesema Chinchibera 

Hassan Sizya ni mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe amewataka wataalam kusaidiana kuhakikisha kuwa maeneo yote yanayopelekewa miradi yanakuwa rafiki ki jeografia ili kupunguza gharama za mradi na kuwezesha kupata majengo mazuri ya viwango vinavyokubalika.

Nae Afisa maendeleo ya Ardhi Wilaya ya Ukerewe Ndugu Paschal Malecha amewataka wananchi wa Ukerewe kuwa tayari kupokea miradi hiyo ya maendeleo yenye manufaa kwa jamii na kuepuka migogoro ya ardhi punde mradi unapoanza kwani migogoro hiyo inachelewesha ukamilifu wa kazi .

"..Tushirikiane kila hatua,tutunze nyaraka zote kuanzia mwanzo mpaka mwisho.." amesema Kaimu Afisa elimu msingi Mwl.Matiko

Nae mkaguzi wa ndani wa Halmashauri hiyo ndugu Majura Kasika amewataka wataalam hao kuwa makini katika matumizi ya mafundi wenyeji "force account" kwa kufuata taratibu ili kuepusha hoja za kiukaguzi wakati na baada ya utekelezaji wa mradi.

Aidha wataalam hao walipata fursa ya kupata elimu ya rushwa kutoka kwa wataalam wa Taasisi ya kupinga na kupambana na rushwa (TAKUKURU) Ukerewe.

Afisa Mkuu wa dawati la elimu kwa umma TAKUKURU (W)Ukerewe Erick Awael Mbise amepiga marufuku kwa wataalam kutengeneza mazingira yoyote yanayoweza kusababisha rushwa na kuwataka kuepuka matumizi mabaya ya fedha.

".. tunahitaji kuona fedha inaonyesha thamani katika miradi inayoenda kutekelezwa.." amesema Mbise

Ikumbukwe kwamba mnamo Juni 30,2025 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ilipokea jumla shilingi Bilioni 2,568,600,000 kutoka serikali kuu kupitia mradi wa BOOST kwa ajili ya ujenzi shule mpya 2, ujenzi wa vyumba vya madarasa, ujenzi wa matundu ya vyoo, ukamilishaji wa maboma sambamba ukarabati wa miundo mbinu mbalimbali ya shule za awali na msingi inayotarajiwa kukamilika Disemba 2025 .

















Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JKT- UKEREWE January 22, 2026
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA MILIONI 9O6.9

    January 19, 2026
  • MFUMO WA SIS KUONGEZA UFANISI SHULENI

    January 14, 2026
  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.