• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

MADIWANI WALA YAMINI TAYARI KUWATUMIKIA WANANCHI

Posted on: December 4th, 2020

Madiwani 36 waapishwa leo tarehe 4 desemba tayari kwa kuanza kazi rasmi ya kuwatumikia wananchi waliowachagua katika uchaguzi Mkuu uliofanyika oktoba 2020, zoezi la kuwaapisha madiwani limefanyika mbele ya Hakimu na kushuhudiwa na Mkuu wa Wilaya pamoja na kamati ya Ulinzi na Usalama, viongozi wa chama, na taasisi za serikali pamoja na umati wa wananchi waliofika kushuhudia tukio hilo la kihistoria kwa miaka mitano ijayo.

Madiwani wote wameapishwa ikiwa ni pamoja na wabunge wawili Mhe. Joseph Mkundi Mhe. Furaha Matondo na kwa kauli moja wamesisitiza juu ya ushirikiano kwani ndio utawezesha wilaya ya Ukerewe kuendelea zaidi.

Aidha mbali na uapishaji wa Waheshimiwa madiwani Baraza limefanya uchaguzi wa nafasi mbili ambazo ni nafasi ya Mwenyekiti wa Halmashauri na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ambapo matokeo kwa nafasi ya Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Joshua Bituro Manumbu amepata kura zote 36 sawa na 100%, nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Athanasi Malobo amepata kura 36 ambazo ni sawa na 100% ya kura zote. Hivyo Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya Josephat Mazula ambaye ndio alikua akiongoza kikao hiko cha uchaguzi amewatangaza viongozi hao.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ndugu Ali Mambile amewapongeza madiwani wote na wabunge kwa kuchaguliwa na wananchi kwa kishindo kikubwa na hii inaonyesha dhahiri kuwa mmeaminiwa na watu katika maeneo yenu. Mambile amewataka kiapo kiende sambamba na kuwatumikia wananchi kwa ueledi na uzalendo mkubwa kwa manufaa ya wilaya yetu.

Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Cornel Magembe ambaye ni mgeni mwalikwa katika kikao hiko amewapongeza sana mwenyekiti wa halmashauri na makamu wake kwa kuaminiwa kuliongoza baraza hilo kwa kipindi cha miaka mitano(5) na amewapongeza madiwani wote amewataka kwenda kusimamia maendeleo katika kata zao kwa kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa katika maeneo yao inakuwa yenye tija kwa wananchi husika na thamani ya fedha inazingatiwa. “sitegemei kuona diwani kubaki nyuma katika kutekeleza miradi ya serikali naamini mtakua mstari wa mbele kusimamia na kuhakikisha tija na ubora wa miradi ili iwanufaishe wananchi” alisema Magembe.

Katibu wa Baraza la Madiwa ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bi. Ester A. Chaula amewapongeza sana madiwani wote kwa kula kiapo cha kuwatumikia wananchi na ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano wakati wote kama ambavyo amekua akifanya katika awamu iliyopita. “nawapongeza sana waheshimiwa madiwani wote Mwenyekiti na Makamu mwenyekiti wa halmashauri kwa kuaminiwa na chama na madiwani kuongoza jahazi hili, ofisi yangu itaendelea kutoa ushirikiano wakati wote nitakuwepo kuwatumikia” aliongeza Chaula.

Mhe Joshua Bituro Manumbu Mwenyekiti wa Halmashauri ameeleza vipaumbele vyake katika kipindi cha uongozi wake ni elimu ambayo itaenda sambamba na kumalizia maabara zote, Maji kuboresha miundombinu ya maji na upatikanaji wa maji wa uhakika, miundombinu ya barabara kuptipika katika misimu yote lakini kubwa ni kuongeza mapato ya halmashauri kwa kubuni vyanzo vipya vya mapato na kushirikiana na wananchi na wadau ili kuona namna ya kupunguza kero za tozo nyingi.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.