• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

MAHAFALI YA KWANZA VETA UKEREWE YAFANA

Posted on: November 24th, 2025

Chuo cha ufundi stadi VETA wilaya ya Ukerewe kimefanya mahafali yake ya kwanza kikihusisha wahitimu wa kada ya ufundi bomba, umeme wa majumbani, ujenzi na ushonaji wa mavazi kwa wahitimu 53 waliohitimu mafunzo hayo kwa mafanikio.

Akizungumza katika mahafali yaliyofanyika katika Chuo cha VETA kilichopo kijiji cha Mlezi kata ya Bukanda Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Cde, Christopher Ngubiagai amewapongeza wahitimu hao huku akisema ujuzi huo utawasaidia vijana hao kujiajiri na kuwaajiri wengine.

" ... tunawapongeza kwa dhati kwa kuwatambua kwamba ninyi ni fahari ya Tanzania, chuo cha ufundi stadi VETA ni sehemu ya jitihada za serikali kuhakikisha vijana wa kitanzania wanapata ujuzi utakaowawezesha kujiajiri na kuajiri wengine lakini pia ni sehemu ya kukuza uchumi wetu..." Cde.Ngubiagai.

Akisoma taarifa Mkuu wa chuo hicho Mhandisi Deusdedith Shinzeh amesema miongoni mwa changamoto kubwa zinazowakabili ni ufinyu wa eneo, upungufu wa maji na muamko mdogo wa wanafunzi kujiunga chuoni hapo hasahasa wazawa .

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ukerewe ambae pia ni Mganga mkuu wa wilaya hiyo Dkt. Charles Mkombe amewasisitiza wazazi na walezi kuendelea kuleta vijana wao katika chuo hicho huku akiahidi kuwa Halmashauri itakuwa bega kwa bega na chuo hicho ili kutatua changamoto zinazojitokeza.

Manyasi Lugembe ni miongoni mwa wazazi wa wahitimu yeye ameeleza kuwa mafunzo ya VETA yamekuwa mkombozi kwa vijana kwa maarifa ya vitendo, na kwamba matokeo wanayoyaona kwa wahitimu yamewafanya wahamasike kwa kusajili watoto wao katika fani hizo.

Anifa Mapesa ni mhitimu wa chuo cha hicho anawapongeza walimu wake kwa kumpa mafunzo mazuri yaliyokuza ujuzi wake katika fani ya uandaaji mavazi huku akisema yupo tayari kufanya kazi na kutengeneza kipato kupitia ujuzi alioupata katika chuo cha VETA Ukerewe.

Akihitimisha kwa kuwatunuku vyeti wahitimu wote Cde.Ngubiagai amewataka wananchi kuendelea kudumisha amani na mshikamano ili kuleta utulivu wa taifa utakaosaidia vijana kusoma kwa amani ili kuzalisha vijana bora watakaokuwa msaada kwa jamii ya Ukerewe na taifa kwa ujumla.


















Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JKT- UKEREWE January 22, 2026
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA MILIONI 9O6.9

    January 19, 2026
  • MFUMO WA SIS KUONGEZA UFANISI SHULENI

    January 14, 2026
  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.