• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

MKURUGENZI MBUA ASISITIZA UKUSANYAJI MAPATO IDARA YA AFYA

Posted on: September 1st, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Ndugu Vincent Augustino Mbua amefanya kikao na wasimamizi wa huduma za afya ngazi ya msingi inayojumuisha waganga wafawidhi,makatibu wa afya,wafamasia,wauguzi wafawidhi, maafisa lishe, maafisa ustawi na wataalam wa maabara kwa lengo la kujitambulisha kwao, kukumbushana maadili ya kazi, kujadili changamoto zinazoikabili idara hiyo sambamba na kutengeneza mlengo wa pamoja katika masuala ya ukusanyaji mapato.

".. Mapato ni kila kitu katika taasisi,tunawajibika kukusanya ili tuweze kujiendesha.Nasisitiza matumizi ya mifumo tuliyonayo na kufunga kamera kwenye baadhi ya maeneo sensitive.."Amesema

Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa upo ushahidi wa ongezeko la mapato kwa kasi katika vituo vya kutolea huduma za afya vinavyotumia mfumo wa GoTHomis na maeneo yaliyofungwa CCTV camera.

Aidha amewataka wataalam hao kutoa huduma bora kwa wateja ikiwa ni sehemu ya maadili ya kazi yao na  kuwavutia wateja wao kujitokeza kwa wingi vituoni kupata huduma za afya huku akiwasihi kuanza kujiponya wao wenyewe afya za akili zao na baadae kusaidia wengine.

Nae Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo Dkt.Charles Mkombe amesema ofisi yake imeandaa utaratibu wa kutoa pongezi kulingana na utendaji kazi wa wataalam wa afya vituoni kwa wote watakaofanya vizuri na watakaofanya vibaya lengo ikiwa ni kuweka hamasa ya ukusanyaji mapato na kuboresha huduma za afya zinazotolewa.

Afisa utumishi Charity Mbirity amewataka watumishi hao kufanya kazi kwa kufuata maadili na kanuni za taaluma yao ya afya na kuwataka waache kujichukulia sheria mkononi kwenye masuala ya matibabu ya msamaha bila kufuata taratibu za kazi.

Akihitimisha kikao hicho Mkurugenzi Mbua amewataka wataalam hao kuachana na tabia zisizofaa kama ulevi uliokithiri huku akiwatia moyo kuendelea kufanya vizuri wakati changamoto zao zikiendelea kutatuliwa .

Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JKT- UKEREWE January 22, 2026
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA MILIONI 9O6.9

    January 19, 2026
  • MFUMO WA SIS KUONGEZA UFANISI SHULENI

    January 14, 2026
  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.