• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

Mkutano wa Wadau wa Maji kwenye Taftishi juu ya kurekebisha bei za Majisafi (NAUWASA)

Posted on: June 22nd, 2017

Wadau wa maji Wilayani Ukerewe wamefanya mkutano ulio andaliwa na EWURA pamoja na  NAUWASA kwa ajili ya Taftishi juu ya maombi ya kurekebisha bei za huduma ya majisafi yanayotolewa na mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Nansio (NAUWASA), Taftishi imefanyika katika ukumbi mkubwa wa Halmashauri ambapo umehusisha wadau mbalimbali ikiwemo baraza la ushauri la watumiaji huduma ya maji na mwakilishi wa ofisi ya Waziri Mkuu na umehudhuriwa na Mkurugenzi Mhandisi Musira Nyirabu pamoja na mmoja wa wajumbe wa bodi ya EWURA Ahmad S.K Kilima, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe Estominh F. Chang’ah ambaye alikua mgeni rasmi, na kaimu Mkurugenzi Mtendaji (W) Moses Nduligu.

Mamlaka ya Majisafi na usafi wa mazingira mjini Nansio (NAUWASA)  ilianzishwa Julai 1,2007 na ilikua na wajibu wa kuhakikisha wananchi wanapata majisafi na salama. Hadi sasa mradi umefanikiwa kujenga mradi mkubwa wa majisafi na usafi wa mazingira uliokamilika mwezi Juni,2016. Mradi ulihusisha ujenzi wa chanzo cha maji na kituo cha kisasa cha tiba Nebuye, ujenzi wa matenki 2 yakiwa na uwezo wa kuhifadhi lita za ujazo 3,350,000.00 kwa pamoja, na mabomba ya usambazaji maji jumla ya kilomita 52.8 na kufanya uzalishaji wa maji kuongezeka kutoka lita 7,000 hadi kufikia 2,500,000 kwa siku.

Changamoto zinazoikabili NAUWASA ni pamoja na gharama kubwa za umeme wa kuazalisha, kutibu na kusukuma maji kwa wateja ambazo zimefikia wastani wa Tsh.18.3 kwa mwezi, gharama hizi ni zaidi ya 96% ya mapato yote ya mamlaka kwa mwezi.

NAUWASA inapendekeza ongezeko la bei kwa wastani wa asilimia 266.50.

EWURA ina jukumu la kudhibiti na kusimamia watoa huduma katika sekta ya majisafi na usafi wa mazingira(ikiwa ni pamoja na sekta ya nishati) pamoja na kudhibiti ubora wa huduma inayotolewa na uhalalo wa bei ya huduma husika.

Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Estominh Francis Chang’ah amefungua mkutano huo na  amewataka wadau kuelewa umuhimu wa huduma ya maji na kuchangia maoini yao ili kuleta maboresho katika huduma inayotolewa na NAUWASA.

Wananchi mbalimbali ambao ndio wadau wakuu wa maji wametoa maoni yao mbalimbali ikiwa ni pamoja na NAUWASA ihakikishe inadhibiti na kuzuia upotevu wa maji hasa mabomba yanayovuja, kuongeza miundombinu na kusajili wateja wapya na kupunguza ukatikaji wa maji.

Mhandisi Goodluck Mmari Katibu Mkuu kutoka Baraza la ushauri la watumiaji wa huduma zinazodhibitiwa na EWURA (EWURA CCC) ametoa maoni mengi baadhi ni pamoja na NAUWASA kuongeza ufanisi wa kiutendaji hii inaenda pamoja na kuongeza masaa ya kutoa hudua kwa siku kufikia masaa 24 tofauti na masaa 12 ya sasa, uwiano wa wateja waliofungiwa dira kiwango cha sasa ni 88% badala ya 100%. Kuondolewa kwa kundi la wateja wasio na mita (unmetered customers) hivyo kusahauri wateja wote wawekewe dira pia wameshauri MWAUWASA kuongeza nguvu kazi kwa kuwa na watumishi wakutosha kulinganisha na sasa ambao 9 wameanzimwa kwa Mkurugenzi Mtendaji(W) na 3 wa MWAUWASA.

Ezamo Sawaki Maponde Mkurugenzi msaidizi kutoka ofisi wa Waziri Mkuu pia amekua na maoni kuwa ongezeko hilo la bei kwa sasa halifai na itakapobidi kuongezwa basi iwe ni hatua kwa hatua, hii inatokana na kuwa chanzo cha maji kipo nan i chanzo cha kudumu NAUWASA ina miundombinu ya kisasa sana lakini 15% tu ya wakazi wa Ukerewe ndio wanapata maji hivyo kunahaja ya kujikita zaidi katika kuimarisha huduma na kuongeza wateja kwa kasi.

NAUWASA imetakiwa kuandika maelezo kwa kina juu ya huduma inayotoa na namna gani wataanza kufanyia kazi mapendekezo na maoni yote yaliyotolewa na wadau wa maji Ukerewe, mabaraza mawili na EWURA ndio majibu yaatarudishwa kulingana na uchambuzi zaidi.

                                                                                Mmoja wa mkazi wa Ukerewe akitoa maoni katika mkutano wa wadau wa maji

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.