• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

MONGELLA APONGEZA HATI SAFI UKEREWE

Posted on: June 4th, 2020


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella amepongeza Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kwa kupata HATI SAFI katika Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa fedha 2018/2019. Ametoa pongezi hizo katika kikao maalumu cha baraza la madiwani kujadili hoja za ukaguzi kikao kilichofanyika ukumbi mkubwa wa halmashauri kilichoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe George Nyamaha na Katibu ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri Bi Ester Chaula na Kuhudhuriwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Katibu Tawala wa Mkoa Emmanuel Tutuba pamoja na wataalamu wa ofisi yake.

Ester Chaula Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Ameliambia baraza la madiwani hali ya hoja zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kufikia mwezi juni 2019 ilikuwa na jumla ya Hoja 93 ambapo kati ya hizo hoja mpya ni 40 na hoja za kipindi cha nyuma ni 53. Utekelezaji wa mapendekezo 93 unaendelea na hadi leo hii mapendekezo 18 yamefanyiwa kazi na hoja zimefungwa na utekelezaji wa mapendekezo 75 yaliyosalia unaendelea. “Katika ukaguzi wa hesabu za serikali mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe imepata HATI SAFI.” Alisema Chaula.

Emmanuel Tutuba Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza amepongeza Halmashauri kwa kufikia mafanikio hayo kwani imekua ni lengo la mkoa kuwa hakuna halmashauri zote ziwe na hati nzuri kwani kupitia kaguzi hizi ni muhimu kwani zinalenga kuhakikisha halmashauri zinakuwa na uadilifu katika matumizi. Pia amewataka wakaguzi wa ndani kufanya wajibu wao ili kusaidia halmashauri kuondokana na hoja za mkaguzi wa nje.

“Nipongeze Baraza lako la madiwani kwa kupata hati safi katika Ukaguzi wa Hesabu za Serikali ikiwa ni baada ya kupata hati za mashaka kwa miaka mnne mfululizo”. alisema John Mongella.

Aidha Mongella amesisitiza bado kama Halmashauri mnatakiwa kuweka utaratibu wa kujadili hoja za Mkaguzi na kuwasilisha kwa mkaguzi wa nje zikiwa tayari na maoni ya kamati ya fedha pamoja na baraza ili kufunga hoja hizo.

Mongella ameitaka Halmashauri kuongeza uwezo wake wa makusanyo ya ndani na kuhakikisha fedha za asilimia 40 zinazotakiwa kwenda katika maendeleo kwani ni takwa la kisheria. Na serikali katika kuimarisha mapato ilianzisha matumizi ya mifumo ya kielektroniki (POS) lakini bado kuna changamoto zilizoainishwa na mkaguzi ya wakusanya mapato kutowasilisha benki kiasi cha Tsh milioni 274, hivyo ameelekeza kamanda wa Polisi Wilaya na TAKUKURU atoa siku saba (7) fedha hizo ziwezimewasilishwa benki na taarifa hiyo iwasilishwe ofisini kwake baada ya siku saba.

Suala la madeni ya madiwani naelekeza kuwa uhakiki ufanyike kwa kushirikiana na ofisi ya RAS nay awe yamelipwa kufikia tarehe 10 juni 2020, na amesisitiza kumbukumbu zote muhimu za kuthibitisha madeni ya waheshimiwa madiwani zitumike na kukamilisha ulipaji mapema iwezekanavyo.

Mhe. George Nyamaha Mwenyekiti wa Halmashauri wa Wilaya ya Ukerewe na diwani wa kata ya Kagunguli amewapongeza kwa namna kila diwani alivyoshiriki katika baraza hilo na kwa kuonyesha ukomavu katika kujenga hoja kwa maslahi ya wanaukerewe.

Nyamaha ameeleza namna serikali ya awamu ya tano imewezesha Ukerewe kuwa na hospitali mbili za wilaya, ujenzi wa madaraja mawili moja Bukungu na kilimabuye, fedha wa ujenzi wa madarasa na nyumba za walimu katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ikiwemo Busangumugu. “ yapo mengi mazuri ambayo Mhe Rais ametekeleza hivyo kwa niaba ya baraza hili natoa shukrani zangu za dhati”.

Aidha amewukuru madiwani wote watendaji wote kwa kufanya kazi vizuri na baraza hilo mpaka kufikia wakati huu, amewatakia heri madiwani wanapojiandaa na mchakato wa kupewa ridhaa katika vyama vyao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.