• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

Ndugulile ahaidi kushughulikia changamoto za hospitali ya wilaya ya Ukerewe

Posted on: July 18th, 2018

Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (MB) Naibu Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto. Akiwa na wataalamu wa wizara ya afya, pamoja na mganga mkuu wa mkoa, amefanya ziara wilayani Ukerewe kwa lengo la kukagua huduma zinazotolewa katika vituo vya afya na hospitali ya wilaya, ambapo ametembelea hospitali ya wilaya ya Ukerewe, vituo vya afya vya Nakatunguru na Kagunguli.

Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Joshua S. Monge ameeleza kuwa mpaka kufikia 2017/2018 kuna jumla ya zahanati 28 za serikali zinafanya kazi na halmashauri imejipanga kufungua zahanati zingine mbili(2) na hii ni katika kutekeleza sera yetu ya kusogeza huduma za afya kwa wananchi. Halmashauri kwa kushirikiana na wananchi imetenga bajeti kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa zahanati katika vijiji vya Buguza, Bukindo, Mibungo, na Nabweko na ujenzi wa nyumba za watumishi katika zahanati za Buguza, Busunda, Nabweko, Bukindo na Mibungo.

Monge ameeleza kuwa upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi katika vituo umeimarika hadi kufikia asilimia 92% katika kipindi cha mwaka 2018. Huduma za afya katika wilaya inakabiliwa na upungufu wa watumishi kwa takribani 76%,kukosekana kwa jengo/kitengo maalumu kwa ajili ya utoaji wa huduma kwa wagonjwa mahututi, upungufu wa stand by genereta, alisema Monge.

Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mhe. Estomihn Chang’ah akimkaribisha Mhe. Naibu Waziri amemweleza jiografia ya wilaya kuwa ni ya visiwa hivyo kunauhitaji wa kuangaliwa kwa jicho la tofauti ilikuweza kuwasogezea huduma ya afya watu waishio maeneo ya visiwani.

Mhe. Joseph Mkundi Mbunge wa jimbo la Ukerewe ameshukuru serikali kwa fedha ilizoleta katika kuboresha miundombinu ya afya ambapo kituo cha afya Bwisya kilipata milioni 400 na ujenzi upo hatua za mwisho na kituo cha afya Muriti kimepokea Tsh. 400,000,000 kwa ajili ya ujenzi/ukarabati ambapo taratibu za awali za ujenzi wa mradi huo tayari zimeanza. Pia kulingana na hali ya kijiografia ya kisiwa chetu cha Ukerewe kunahaja ya kuwa na boti ya wagonjwa wa dharura (ambulance boat) itakayohudumia wagonjwa wadharura tuu kuwapeleka hospitali ya wilaya au mwanza ambapo kuna hospitali kubwa zaidi. Alisema Mkundi.

Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (MB) Naibu Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto akizungumza katika ziara hiyo amepongeza uongozi wa halmashauri na wilaya kwa kuwa na mpangilio mzuri, usafi na utoaji mzuri huduma katika hospitali ya wilaya na vituo vya afya kwani malalamiko yamepungua kwa kiasi kikubwa.

Ndugulile amefanya ziara hii wilayani Ukerewe baada ya Mbuge wa Ukerewe Mhe. Mkundi kuwasilisha bungeni hali ya huduma ya afya na changamoto ya kijiografia ya kisiwa kuwa na changamoto nyingi. Akitoa majibu ya changamoto zinazoikabili halmashauri katika sekta ya afya ameahidi kushughulikia suala la upatikanaji wa vifaa vitakvyowezesha kufunguliwa na kuanzishwa kwa huduma ya wodi ya wagonjwa mahututi, huduma ambayo hivi sasa haipo na ni huduma muhimu kwa wananchi wa kisiwa cha Ukerewe. Hivyo amewataka kutenga jengo litakalotumika kwa wagonjwa mahututi. Pia ameahidi kushughulikia suala la upatikanaji wa watumishi wa afya kwani itasaidia kuondoa upungufu unaoikabili hospitalinya Wilaya, vituo vya afya na zahanati.

Ndugulile amewataka usimamizi ufanyike kwa ukaribu katika maeneo ambayo serikali imetoa fedha kwa ajili ya kuwasogezea huduma wananchi na kuwa lengo hilo limefikiwa. 

  

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.