• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

SHULE ZA MSINGI UKEREWE ZIMEPOKEA VITABU 38,891

Posted on: August 7th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Ndg. John Mongella amefanya makabidhiano ya vitabu 38,891 vitakavyoenda kutumika katika shule za msingi kote wilayani ukerewe. Makabidhiano ya vitabu kwa Maafisa Elimu kata na Walimu wa kuu waliojitokeza katika eneo la kituo cha waalimu kujifunzia (TRC).

Afisa Elimu Msingi Reginald Richard akizungumza wakati wa makabidhiano hayo ameeleza Wilaya ya Ukerewe ina jumla ya Wanafunzi 108,812 wavulana wakiwa 54,820 na wasichana 53,992 kuanzia awali hadi darasa la saba. Wilaya ilikuwa na upungufu mkubwa wa vitabu hasa vya darasa la nne hadi kufikia uwiano wa kitabu kimoja kwa wanafunzi watano. Hali ya elimu inaenda inabadilika kutoka walipokuwa kwani mwaka 2017 walifaulu kwa 52.7% lakini kwa mwaka 2018 kwa matokeo ya Mock yaliyotoka mwezi huu mwanzoni wamepanda kwa 61.5%. “Baada ya kupokea vitabu hivi uwiano wa kitabu kimoja kwa wanafunzi watatu ingawa lengo la serikali ni kufikia uwiano wa kitabu kimoja kwa mwanafunzi mmoja” alisema Richard.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Ndg. John Mongella amepongeza jitihada zinazoendelea kufanywa na Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe katika kunyanyua hali ya elimu katika wilaya ambayo inazidi kuboreka kadri siku zinavyokwenda. Amewataka walimu wa kuu kuendelea kusimamia vema walimu kutimiza wajibu wao vizuri na kuifanya wilaya upate ufaulu wa juu zaidi na kutumia vitabu hivyo kama nyenzo muhimu katika kufikia malengo ya elimu katika mkoa wa mwanza.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Ndg. Frank S. Bahati ameishukuru Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Wizara ya Elimu kwa kuendelea kuboresha hali ya elimu hasa katika Wilaya ya Ukerewe kwa kuleta vitabu 38,891 vitakavyoenda kuwa chachu ya ufaulu kwa wanafunzi na hivyo kunyanyua kiwango cha ufaulu. “Tunaishukuru Serikali kwa kutuletea vitabu ilikupunguza tatizo la upungufu wa vitabu katika shule zetu za Msingi” alisema Bahati.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.