• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

TASAF MKOMBOZI WA WANYONGE

Posted on: July 11th, 2025

Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) Ukerewe kupitia mradi wa kunusuru kaya maskini umekamilisha zoezi la uhawilishaji fedha kwa dirisha la kipindi cha Machi - Aprili 2025 ambapo jumla ya kiasi cha shilingi milioni 362,517,000 kimetolewa kwa kaya 5,723 ndani ya Wilaya ya Ukerewe.

TASAF Ukerewe imekuwa na utaratibu wa kutoa elimu mbalimbali za msingi za kijamii kwa walengwa ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha wahusika wanaelewa matumizi bora ya kipato chao na kuimarisha mazingira ya maisha yao ya kila siku.

Aziz Makongo ni muwezeshaji kutoka TASAF Ukerewe amewataka walengwa wa TASAF wa kijiji cha Nkilizya kilichopo kata ya Nkilizya kujitathimini juu ya mafanikio waliyoyapata kwa kipindi chote cha mradi.

"..Ni wakati wa kutafakari kuhusu mafanikio hadi sasa ,kitu ambacho kitatusaidia kujua tulipotoka na tulipo.."

Maboga Bega ni mlengwa wa TASAF katika kijiji hicho cha Nkilizya yeye anasema mradi umemsaidia kukua kiakili kwa kuwa ameweza kukutana na wenzake wengi ambao wamekuwa wakiongea mara kwa mara nini wafanye angalau wakuze kipato chao na kujikwamua na umaskini uliokithiri.

"..Tumefanikiwa kuunda vikundi vya kuweka akiba na kukopeshana,kwa kiasi flani mradi huu umenifundisha kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha,niseme tu TASAF ni mkombozi wa wanyonge.." amesema Maboga

Nae Mratibu wa TASAF Wilaya ya Ukerewe Bi.Jenitha Damaseni amewaweka wazi walengwa hao kuhusu ukomo wa mradi wa kunusuru kaya za walengwa (PSSN II) ifikapo Septemba 2025.

".. Tunataka kuhakikisha kuwa mpo tayari kuendelea na maisha hata baada ya mpango na kusherekea mafanikio mliyoyapata hata kama ni madogo angalau yameweza kukuvusha kutoka hatua moja hadi nyingine.."

Sophia Mataba ni mlengwa wa mpango huo katika kijiji cha Bukongo yeye anasema TASAF imemsaidia kujiimarisha kiuchumi.

"..Nilianza bila kitu baadae nikanunua mbuzi wawili baada ya mwaka wakaanza kuzaliana nikaanza kuuza kwa ajili ya kupata pesa ya matumizi ya nyumbani mpaka sasa nimebaki na mbuzi saba.Pia nina wajukuu wanne ambao wote wanahudumiwa na TASAF kiafya na kielimu.." 

Akihitimisha zoezi hilo katika kijiji cha Nkilizya mwenyekiti wa kijiji hicho Alphaxard Pima amewaasa walengwa wote kufuata yote waliyofundishwa na kudumu katika vikundi vya kuweka akiba na kukopeshana na kuimarisha upendo baina yao.

Uhawilishaji huo umefanyika kwa njia ya utoaji fedha taslim  ambapo milioni 123,563,000 zimetolewa kwa walengwa 1,786 na kiasi cha shilingi milioni 248,954,000 kimewekwa kwenye akaunti na mitandao ya simu za walengwa 3,935.

















Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • UKEREWE YAANZA RASMI UTEKELEZAJI WA MRADI WA BOOST

    July 25, 2025
  • WATUMISHI IDARA YA AFYA WAASWA KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA MAADILI

    July 23, 2025
  • MKURUGENZI MBUA ASISITIZA MATUMIZI BORA YA MIFUMO YA SERIKALI

    July 22, 2025
  • WALIMU WAELEWESHWA DHANA YA UTHIBITI UBORA WA SHULE

    July 22, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.