• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

UADILIFU NA UWAJIBIKAJI KWA WALIMU NI NGUZO YA MAFANIKIO

Posted on: December 3rd, 2025

"... uadilifu ni nguzo ya kuaminika na kufanikiwa walimu wakuu muwajibike  kuwajenga walimu na wanafunzi katika masuala ya kusimama imara katika shughuli zao za kila siku kuepuka rushwa katika kusimamia utoaji bora wa elimu, kuzuia utoro na vitendo visivyofaa ili kuleta maendeleo katika jamii..." 

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Cde, Christopher Ngubiagai katika mkutano wa tatu wa Umoja wa walimu wakuu wa shule za msingi Tanzania bara (TAPSHA) Ukerewe uliopambwa na kauli mbiu " mtaala ulioboreshwa kwa elimu bora ujuzi na ubunifu kwa maendeleo endelevu ya taifa" uliofanyika katika ukumbi wa Millenium Plaza kata ya Nansio Ukerewe.

Cde.Ngubiagai amewataka walimu hao kuwa wasikivu na wazalendo kutumia vipawa na vipaji vya wale wanaowaongoza huku akiwasisitiza kujitoa kwa ajili ya jamii na kuwalinda na kutengeneza mazingira wezeshi kwa wanafunzi wanaotoka kwenye mazingira magumu.

Akisoma risala katibu Mkuu wa TAPSHA Ukerewe Mwalimu Fadhili Usufu amesema umoja huo umefanikiwa kupunguza idadi ya wanafunzi wasiomudu Kusoma,kuandika na kuhesabu (KKK), usimamizi wa miradi, kutoa msaada kwa wahitaji na kutoa motisha kwa shule zilizofanya vizuri kwa matokeo ya kumaliza elimu ya msingi.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ukerewe ndugu Vincent Mbua amewasihi walimu hao kushirikiana na wataalam nyakati zote hasa hasa wakati wa kufanya malipo ya miradi na kuwa waangalizi wa miundombinu ya shule huku akikiri kutambua uhaba wa watumishi ndani ya Halmashauri yake ikiwemo sekta ya elimu.

Nae Afisa elimu msingi Mwalimu Bahati Mwaipasi amewapongeza walimu kwa utendaji kazi thabiti uliosaidia kuongeza ufaulu kutoka 82% mwaka 2024 hadi asilimia 87 mwaka 2025 katika mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi huku akisisitiza suala la uchangiaji chakula shuleni kuwa muhimu kwa wanafunzi kufanya vizuri kitaaluma.

 Cleophace Majige ni mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kulazu yeye anashauri walimu kuyafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na viongozi ili kuendeleza jitihada za kutengeneza wataalam wazuri watakao litumikia taifa .

Mhe.Ngubiagai amewataka walimu hao kulinda amani, kuishi kwa umoja na mshikamano,kukemea lugha za chuki,dharau na ubaguzi na kuzifanya shule kuwa eneo rafiki la undugu kwa kujenga malezi bora kwa wanafunzi .


















Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • UADILIFU NA UWAJIBIKAJI KWA WALIMU NI NGUZO YA MAFANIKIO

    December 03, 2025
  • DC NGUBIAGAI AWAASA VIJANA KULINDA AMANI

    December 01, 2025
  • AGENDA YA LISHE IWE YA KUDUMU

    December 01, 2025
  • WATOA HUDUMA ZA CHANJO 66 WAPATIWA MAFUNZO KUIMARISHA HUDUMA HIZO

    November 28, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.