• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

UFUNGUZI WA OFISI YA PSPF UKEREWE WAPOKELEWA KWA KISHINDO

Posted on: October 3rd, 2017

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambaye ni Katibu Tawala msaidizi Elimu ndugu Michael Ligola amewasili wilayani Ukerewe pamoja na mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu PSPF Gabriel Silayo pamoja na uongozi wa Wilaya ya Ukerewe wameshiriki katika hafla ya ufunguzi wa ofisi ya Mfuko wa pensheni kwa wafanyakazi. Hafla hiyo imefanyika katika eneo la ofisi za maliasili zamani mjini Nansio na kuhudhuriwa na wananchi na watumishi wa serikali.

Chacha Naikabwe Meneja PSPF Mkoa wa Mwanza na Mara amewasilisha mada juu ya PSPF (Public Service Pension Fund) ilianzishwa kwa mujibu wa Sheria namba 2 ya mwaka 1999 iliyotokana na sheria ya mwaka 1954 ikiwa na majukumu kama kutambua na kusajili wanachama, kuwekeza michango inayokusanywa,kukusanya michango kutoka kwa mwajiri 15% na 5% mtumishi, kulipa mafao, kutunza kumbukumbu za wananchama na kutoa elimu ya mafao.

Gabriel Silayo mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu PSPF ameeleza kuwa imekua ni jambo jema Ukerewe kupata ofisi kwani ni eneo leny changamoto ya kijiografia na kuna wanachama wanaochangia hivyo ameahidi kuwa ofisi hiyo itatoa huduma njema bila kupata adha ya kwenda Mwanza. Silayo ameeleza kuwa wilaya ya Ukerewe imepata upendeleo kuwa kati ya miongoni mwa Wilaya chache zilizobahatika kupata Ofisi ikiwemo Pemba, Zanzibar na sehemu nyingine,  kwani kwa sasa ofisi zipo katika ofisi za mkoa wa Mwanza.

Michael Ligola Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza akitoa hotuba amepongeza sana Mfuko wa PSPF kuwa mfuko wa kwanza kufungua na kusogeza huduma za ofisi katika wilaya ya Ukerewe ili kuweza kupata huduma kwa karibu kama wanavyoweza kupata watanzania wengine. Kwa maana hiyo inatekeleza kwa vitendo kaulimbiu ya PSPF pamoja nawe. “Nina imani kuwa huduma zote za mfuko zitapatikana Ukerewe” Ligola. Ametoa rai kuwa mfuko utoe elimu ya kutosha kwa wananchi juu ya mifumo miwili ya uchangiaji yaani ule wa uchangiaji wa hiari kwa wananchi wote na ule wa sekta za ajira rasmi. Hivyo amewataka wananchi wa Ukerewe kuchangamkia fursa ili kunufaika na mafao na huduma za PSPF.

Ligola amewataka waajiri kuchangia watumishi wao kwa wakati ili kuwaepushia wale watakao kuwa wakistaafu kushindwa kulipwa mafao yao, hivyo amesisitiza kuwa ni swala baya kwani ni kuwatesa wastaafu pasipo sababu. Kauli mbiu ya Mfuko wa pensheni wa PSPF katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja mwaka huu ni Tunasikiliza Tunakujali, PSPF pamoja nawe. 


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.