• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

UJENZI KITUO CHA AFYA BWISYA WAFIKIA 95%

Posted on: July 7th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella amefanya ziara ya siku moja katika kisiwa cha Ukara Wilayani Ukerewe lengo likiwa kukagua maendeleo katika sekta ya afya na elimu.katika ziara hiyo ametembelea na kukagua ujenzi wa kituo cha Afya Bwisya na shule ya sekondari Nyamanga.

Kituo cha Afya Bwisya ni kituo kinachojengwa kwa fedha zaidi ya milioni 800 ambazo Mhe. John Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alielekeza zijenge majengo hayo baada ya fedha hiyo kubaki baada ya rambirambi kutolewa. Usimamizi wa maelekezo hayo ambapo mpaka sasa ujenzi wa kituo cha afya Bwisya uko vizuri na umefika 95% na asilimia zilizosalia zitakamilishwa ndani ya siku chache zijazo. Alisema Mongella.

Mongella ametoa rai kuwa kasi ya kukamilisha usafi na shughuli zingine za mwisho iongezeke ili wananchi waanze kupatiwa huduma kwa ukamilifu.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella ametembelea pia Shule ya Sekondari Nyamanga ambayo inajengwa katika kata ya Nyamanga katika eneo ambalo wanafunzi walikua na adha kubwa ya kutembea umbali mrefu kufuata masomo katika shule za sekondari za Bwisya na Bukiko. Hatua ya ujenzi wa shule hiyo ya Nyamanga ni jambo la faraja ambapo wanafunzi wameanza kusoma katika shule hiyo.

Ukamilishaji wa majengo katika shule hiyo bado unaendelea ambapo maabara na baadhi ya madarasa yapo katika hatua ya kunyanyua boma.

Mongella amewataka watendaji kuongeza kasi katika ujenzi huo kwani shule hiyo ni mkombozi kwa anafunzi waishia Nyamanga na vijiji vya karibu.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella ameeleza kuwa ujenzi wakivuko kikubwa kitakacho tumika kuvusha watu mizigo na magari kwenda Ukara kinaendelea kuundwa na SONGORO MARINE na kinatarajiwa kuwa kikubwa chenye uwezo wa kubeba gari 20 na abiria zaidi ya 1000.

Ester A. Chaula Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe amesema ujenzi wa kituo cha afya na shule ya sekondari Nyamanga ni muhimu kwani wananchi wa kisiwa cha Ukara watapata huduma bora katika sekta ya elimu na afya. Ameahidi kuhakikisha ukamilishaji utafanyika kwa ubora.

Cornel Magembe Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe amepongeza na kushukuru serikali ya awamu ya tano kwa kuiletea Ukerewe maendeleo kwani Serikali inawajali watu wake.

Napenda kukukaribisha Wilaya yetu ya Ukerewe hasa katika kisiwa cha Ukara kuona na kufungua kituo kikubwa cha afya Bwisya ambacho kitakua msaada mkubwa kwa wananchi wote wa tarafa ya Ukara na vijiji vya karibu. Alisema Magembe.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.