• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

UKEREWE WAADHIMISHA SIKU YA UHURU KWA KUPANDA MITI.

Posted on: December 8th, 2021

Katika kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya Ambaye ni Katibu Tawala wa Wilaya Bi. Zubeda Kimaro akiwa na kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, wakuu wa Idara na vitengo, wakuu wa taasisi mbalimbali, viongozi wa chama, kata, kijiji na wananchi wamejitokeza na wameshiriki zoezi la upandaji Miti 680 katika shule mpya ya wasichana Ukerewe iliyopo kata ya kagunguli Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza kwa lengo la kuhifadhi mazingira na kuadhimisha miaka 60 ya Uhuru. 

Akizungumza na wananchi waliojitokeza kushiriki zoezi hili katika eneo la Shule ya wasichana Ukerewe iliyopo kata ya Kagunguli wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza, Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Bi. zubeda Kimaro amewaagiza viongozi walezi wa kata zote kusimamia zoezi la upandaji miti katika taasisi za serikali zilizo katika maeneo yao ili kufikia lengo la kupanda Miche elfu tano kwa Wilaya nzima ya Ukerewe.

Aidha, Bi. Zubeda amewaomba wananchi kushiriki zoezi la kupokea chanjo ya uviko 19 linalo endelea kutolewa wilayani hapo na kufafanua kuwa chanjo hiyo ni salama na haina madhara yoyote kwa mwananchi.


Kwa upande wake Afisa Misitu Wilaya ya Ukerewe Goodluck Mtigandi ameeleza kuwa, kwa kipindi cha miaka mitano  iliyopita halmashauri ya wilaya ya Ukerewe imefanikiwa kupanda miti laki mbili, hamsini na saba elfu na mia tano katika hekta elfu mbili kumi na saba tu, miti hiyo imepandwa katika hifadhi za serikali, Misitu ya jamii, taasisi za umma pamoja na maeneo ya watu binafsi miti ambayo imetolewa na TFS.


Kwa mwaka 2021 halmashauri ya wilaya ya Ukerewe imepanda jumla ya miti laki moja arobaini na moja elfu katika maeneo mbalimbali Wilayani hapo.


Afisa Misitu Mtigandi ameelezea mpango wa halmashauri kwa mwaka 2021 kuwa inatarajia kupanda hekta mia tisa tisini na saba katika maeneo ya wilaya nzima hasa maeneo yasiyo na miti katika kisiwa kikubwa cha Nansio, Kisiwa cha Ukara, kisiwa cha Irugwa na kisiwa cha Bwiro ikiwa ndiyo maeneo yaliyopewa kipaumbele.

Aidha Bi. Zubeda ameshukuru Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) Hapa Wilayani Ukerewe na Shamba la miti Rubya kwa juhudi wanazozionesha kuhakikisha miti mingi inaendelea kupandwa katika Wilaya ya Ukerewe na utoaji wa Elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa Miti na utunzaji mazingira.

KAULIMBIU "Miaka 60 ya Uhuru, Tanzania imara na kazi iendelee".

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • " UMOJA NA USHIRIKIANO NDIO NGUZO YA MAFANIKIO ." -SHEREMBI

    June 28, 2025
  • MASHIRIKI YASIYO YA KISERIKALI YAMEASWA KUFANYA KAZI KWA KUFUATA MISINGI INAYOFAA

    June 27, 2025
  • BILIONI 39 KUJENGA HOSPITALI YA RUFAA KATA YA BUKINDO

    June 25, 2025
  • " TUDUMISHE AMANI YETU." - DC NGUBIAGAI

    June 24, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.