• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

WADAU WA KILIMO CHA MACHUNGWA WAPIGWA MSASA UKEREWE.

Posted on: September 11th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Mhe.Cornel Magembe ahamasisha kilimo cha machungwa kwa wakulima wa Wilaya hiyo kwani ni moja ya kilimo biashara chenye tija kuanzia kwa mkulima hadi taifa, ameyasema hayo akifungua mkutano wa wadau wa machungwa, katika Ukumbi wa Albino ulioandaliwa na MVIWAU chini ya ufadhili wa VI Agroforesty na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. George Nyamaha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Ester Chaula, waheshimiwa madiwani, wakuu wa Idara na taasisi za kifedha.

Magembe ametoa rai kwa wakulima na wadau  hao kufuata kanuni na taratibu muhimu za kilimo hiko cha machungwa ili kuweza kupata mazao bora na ya kutosha. Amesikitishwa na uuzaji wa machungwa ambayo bado matunda hayajakomaa na kufanya hivyo inaumiza mkulima. Baadhi ya kanuni na taratibu hizo ni utunzaji wa mimea hiyo uchaguzi wa mbegu bora na ushirikishwaji wa wataalamu wa kilimo juu ya uangalizi wa mimea hiyo.

Magembe amewataka maafisa ugani kutokaa maofisini tu bali kutoka na kusambaa sehemu mbalimbali katika kata zao ili kutoa ushauri wakitaalamu juu ya kilimo na kuwezesha kilimo bora kitakachoweza kukidhi haja ya mkulima kiuchumi na kuongeza chachu ya maendeleo ya wilaya. “Serikali itahakikisha kuzidisha mchango wake katika sekta ya kilimo”.Alisema Magembe katika mkutano huo na kuzidi kuhamasisha kwamba si mimea ya michungwa pekee bali hata mimea ya matunda mengine ili kukidhi haja ya viwanda vya Tanzania na wawekezaji kwa ujumla.

Magembe pia amekemea tabia ya wakulima hao ya kuuza miche michanga ya mimea ya michungwa bila kuangalia faida ya mbeleni ya uzao wa mimea hiyo na matokeo yake kuiuza kwa bei ya chini sana na kupelekea kudumaa kiuchumi .Hivyo amehakikisha kukomesha tabia hiyo ya wakulima na kushauri zao hilo kuwa zao la biashara wilayani humo.

Kent Larsson Meneja Mkazi wa Shirika la VI Agroforesty lenye makao yake makuu nchini Sweden ambao ni wafadhili wa Shirika la Muungano wa Vikundi vya Wakulima, Wavuvi na Wafugaji Ukerewe (MVIWAU), amesema Shirika hilo limeonesha mchango wake katika kilimo ikiwa na utoaji bure wa elimu ya kilimo,ushauri wa mbegu bora za mimea ya bustani hususani michungwa ikiwa  lengo lao kubwa mbali na kupiga vita umaskini wa wakulima bali pia ni kuiunga mkono serikali katika kilimo cha mimea ya matunda wilayani humo kupitia miradi mbalimbali kama ALIVE [Agoforesty For Livelihood Empowerment]ulioanzisha wilayani humo.

Larsson ameeleza kuwa uboreshwaji wa fursa mbalimbali kwa wakulima ili kuboresha kilimo cha zao la machungwa na matunda kwa ujumla ili kuwakwamua wakulima kiuchumi na kuboresha maisha ya wananchi hasa wakulima wa Ukerewe.

Aidha mashirika ya kifedha na vikundi mbalimbali kama NMB Bank [National Microfinance Bank] na Ukerewe SACCOS yameonyesha mchango mkubwa kwa wakulima kwa kuwawezesha mikopo ili kuendeleza kilimo bora na chenye tija.

Wakulima katika mkutano huo wameiomba Halmashauri ya wilaya hiyo kuimarisha mipango mikakati ya biashara na kilimo kwa ujumla ili kuimarisha kilimo cha machungwa kilicho bora na kukidhi uchumi wa wakulima na jamii za Wakerewe kwa ujumla.

Paulin Makubi Mwenyekiti wa MVIWAU ameshukuru shirika la VI Agroforesty kwa kuendelea kushika mkono kilimo katika Wilaya ya Ukerewe, pia ameshukuru Halmashauri kwa kuendelea kutoa ushirikiano. Ameomba wakerewe kuanza kujihususha na ufugaji wa samaki ndani ya ziwa kwani ni chanzo kizuri cha uchumi.

Gregory K. Gabriel, Diwani wa kata ya Bukindo na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe  amewataka wakulima wa machungwa kufanyia kazi maelekezo na ushauri wa wataalamu wa kilimo na kuongeza tija na thamani katika kilimo cha matunda, amewapongeza na kuwashukuru shirika la VI Agroforesty kwa kuendelea kujali uchumi wa ukerewe kwa kutoa mafunzo na fursa za kilimo hasa machugwa na upandaji miti kwa zaidi ya miaka 20 sasa kwani imesaidia utunzaji wa mazingira kwa kiasi kikubwa.Amesema hayo wakati wa kufunga mkutano huo wa wadau wa kilimo cha machungwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.