• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUANZA KLINIKI MAPEMA

Posted on: September 18th, 2025

Kina mama wajawazito Wilayani Ukerewe wameshauriwa kuwahi Kliniki punde wanapojigundua na kuona dalili za ujauzito ili kupata vipimo, ushauri na dawa kinga muhimu kwa ajili ya ukuaji mzuri wenye afya kwa wote mama na mtoto.

Akitoa elimu wakati wa Kliniki ya Baba, Mama na Mtoto Muuguzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe (Bomani) Jesca Majura amewahimiza akina mama waliofika kliniki kwa ajili ya huduma mbalimbali kuanza mapema kliniki kwa kuzingatia umuhimu na faida nyingi zinazopatina .

".. inasaidia kufahamu afya ya mama na mtoto, kupata huduma za mapema kama chanjo, vipimo, ushauri, dawa kinga na matibabu ya haraka pale inapolazimu kufanya hivyo hali inayomuwekea mama mazingira rafiki ya kujifungua salama mtoto mwenye afya.

Aidha amewaasa wajawazito kupata matibabu ya magonjwa ya zinaa kama Kaswende, Maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi na Malaria kwani ni magonjwa yanayoweza kumuathiri mtoto akiwa tumboni au wakati wa kuzaliwa huku akiwasihi kina mama hao kuachana na imani potofu pale mtoto anapozaliwa na changamoto ya kichwa kikubwa au mgongo wazi kwa kutambua hayo ni miongoni mwa madhara ya mama mjamzito kuchelewa kuanza kliniki .

Salome Mathiasi Mchele ni mkazi wa kijiji cha Bukongo kata ya Bukongo yeye amepongeza utolewaji wa elimu hiyo kwa wazazi kwani imewawezesha kufahamu kuwa hata vyanzo vingi vya vifo vya watoto wachanga vinatokana na mama mjamzito kuchelewa kuanza huduma za kliniki hiyo.

"..Muende mkawe mabalozi wazuri huko majumbani na muwasisitize wamama waje mapema ,zipo dawa kinga ambazo mama anaweza kutumia pale anapotaka kupata ujauzito ambazo zitamkinga na maradhi na atakuwa salama mpaka kujifungua.."

Doris Elias mkazi wa kijiji cha Kagera anasema amenufaika na elimu hiyo na kwamba hatokosa kliniki hata siku moja ataenda na ratiba zitolewazo na wauguzi kwani anatamani kupata mtoto mwenye afya nzuri.amewaomba wazazi wote kuzingatia Kliniki na kufuata utaratibu wote kwa mujibu wa ratiba zitolewazo na wauguzi hospitalini hapo.

Akihitimisha elimu hiyo Jesca Majura amesema hakuna sababu yakuruhusu mama mjamzito apate changamoto zinazoweza kuzuilika kwa kuwahi kliniki.

















Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI 2025 September 03, 2025
  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI AKABIDHIWA MELI YA MV BUTIAMA KUANZA KAZI RASMI

    September 20, 2025
  • JAMII TUNAWAJIBIKA KULINDA AMANI YETU - DC NGUBIAGAI

    September 19, 2025
  • WAJAWAZITO WASHAURIWA KUANZA KLINIKI MAPEMA

    September 18, 2025
  • MAFUNZO YA KANUNI NA MIONGOZO UENDESHAJI ZOEZI LA UTOAJI MIKOPO YA 10% YAZINDULIWA RASMI

    September 12, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.