• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

WALIMU WAKUU WATAKIWA KUIMARISHA UMOJA NA MSHIKAMANO

Posted on: December 11th, 2025

Walimu wakuu wateule wametakiwa kuimarisha umoja na mshikamano kwa watu wanaokwenda kuwaongoza, lengo la kikao hicho ilikuwa kuwakumbusha walimu hao kuhusu maadili, mahitaji ya mtaala mpya na miongozo juu ya utendaji kazi katika vituo walivyopangiwa.

"... nendeni mkaimarishe umoja na mshikamano kwa kundi mnalokwenda kulisimamia, mkaboreshe kwenye mapungufu mkawe makini katika kufanya maamuzi yatakayoleta manufaa kwa jamii inayowazunguka..." Amesema Rasuli Amir Mbwambo- Kaimu Afisa elimu msingi. 

Kwa upande wake Afisa uthibiti ubora wilaya ya Ukerewe Mwl. Misana Nyasani Maige amewataka walimu hao kuzingatia maelekezo ya mtaala mpya wa elimu ikiwa ni kuwa na Mihitasari, miongozo ya ufundishaji, vitabu vyenye ithibati, maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, shajala ya masomo, shajala ya vipindi na kuunda vyama vya masomo kupitia idara ya ndani ya uthibiti ubora vitakavyowaongezea weledi katika utendaji .

Nae Katibu msaidizi tume ya utumishi wa walimu Mwl. Richard Edward Shaban amewasihi walimu hao kujibidisha kufahamu kanuni, miongozo na sheria ambazo zitawasaidia kuwaongoza katika kusimamia maadili na nidhamu kwa kundi wanalokwenda kulisimamia huku akiwataka kujiweka kando na masuala ya utovu wa nidhamu ili kulinda heshima zao kama viongozi.

Mwalimu Luchagula Masanja ni mwalimu mkuu wa Shule ya msingi Bukiko amewasihi walimu wenzake kushirikisha walimu wao katika mambo mbalimbali kwa ajili ya kutanua uelewa na kuondoa tofauti zinazoweza kujitokeza huku akiwaomba kuendana na mazingira ili kurahisisha utendaji kazi.

Akihitimisha kikao hicho Mbwambo amewataka walimu hao kuiunganisha jamii na taasisi, kutengeza motisha zitazowavutia walimu wengine kujiunga na shule zao huku akiwaasa kuongeza umakini katika kusimamia miradi na vifaa vinavyotolewa na serikali katika shule wanazoziongoza ili kuleta maendeleo katika taasisi hizo.

Jumla ya walimu wakuu 15 wameteuliwa.


















Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA USAILI December 05, 2025
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WALIMU WAKUU WATAKIWA KUIMARISHA UMOJA NA MSHIKAMANO

    December 11, 2025
  • MAPATO YA NDANI NI UTI WA MGONGO WA HALMASHAURI YETU - MHE.MAZIGE

    December 05, 2025
  • WALIMU WAASWA KUWA WABUNIFU NA WASIKIVU

    December 04, 2025
  • UADILIFU NA UWAJIBIKAJI KWA WALIMU NI NGUZO YA MAFANIKIO

    December 03, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.