• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

WANANCHI UKEREWE WAASWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU

Posted on: August 1st, 2025

Katibu tawala wa mkoa wa Mwanza ndugu Elkana Balandya amewaasa wananchi wa wilaya ya Ukerewe kujiandaa kushiriki uchaguzi mkuu utakaohusisha uchaguzi wa madiwani, wabunge na Rais unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2025 kwani ndio njia pekee ya kupata viongozi wanaowataka.

Amezungumza hayo katika maeneo tofauti wakati alipokuwa katika ziara ya siku moja akiongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Mwanza kwa ajili ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani humo.

".. kushiriki uchaguzi ni haki ya msingi ya kila mwananchi,muhamasishane mjitokeze kwa wingi mchague viongozi kwa maslahi yenu.."

Ndugu Balandya ametoa pongezi kwa serikali ya awamu ya sita kwa kazi nzuri inayoendelea ya kufanya maboresho makubwa katika sekta ya elimu,afya, maji,miundo mbinu na barabara. 

Aidha akiwa mradi wa ujenzi wa bweni la wasichana katika shule ya sekondari Ukerewe iliyopo kata ya Kagunguli  ndugu Balandya amewataka wanafunzi katika shule hiyo kuwa mstari wa mbele katika masuala ya kupinga rushwa kwani ni adui wa haki na kuachana kabisa na matumizi ya dawa za kulevya ambazo ni hatari kwa afya zao.

Rahma Kagembe ni dada mkuu katika shule hiyo yeye amesema wanaelewa kuhusu rushwa na wajibu wao mkubwa ni kuhakikisha wanasoma kwa bidii ili kufikia malengo waliyojiwekea.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo ndugu Vincent Augustino Mbua  amesema amepokea maelekezo yote yaliyotolewa katika kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati na kwa viwango vya ubora vinavyotakiwa .

Miradi mingine iliyotembelewa ni kituo cha afya Kigara kwa fedha kutoka serikali kuu, ujenzi wa hoteli na maduka ya biashara kwa fedha za mapato ya ndani sambamba na barabara ya Sungura.

















Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JKT- UKEREWE January 22, 2026
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA MILIONI 9O6.9

    January 19, 2026
  • MFUMO WA SIS KUONGEZA UFANISI SHULENI

    January 14, 2026
  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.