• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU WANUFAIKA NA MILIONI 71 UKEREWE

Posted on: January 24th, 2020

Baraza la Madiwani linaloongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe George Nyamaha Diwani wa Kata ya Kagunguli (CCM) na Makamu Mwenyekiti Gabriel Kalala Gregory Diwani wa Kata ya Bukindo (CCM) wamekabidhi hundi kwa vikundi 24 vilivyoomba mikopo hiyo kwa shughuli mbali mbali za kiuchumi, jumla ya thamani ya hundi hizo ni Tsh 71,000,000/= .

Nyamaha amewapongeza vikundi hivyo kwa kupata mikopo hiyo na amewataka kutumia vema na kurudisha kwa wakati ili wengine waweze kukopeshwa kama wao walivyopata. Ni dhamira yetu kuhakikisha wananchi wa Ukerewe wanaweza kufanya na kujishughulisha katika kujiingizia kipato.

Innocent Gitubabu Maduhu Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ukerewe amesema fedha hizo zimetolewa kwa lengo la kuwainua kiuchumi kwani vikundi vyote 24 vilivyoomba vinashughuli za kiuchumi na wanapaswa kurejesha kama walivyoelekezwa. Pia kuwajengea vijana, walemavu na wanawake uwezo wa kujitegemea. “Ugawaji wa mikopo hii ni kutekeleza sera ya serikali ya kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri ili kukopesha wanawake, vijana na walemavu”. Alisema Maduhu.

Cecilia Oswago Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii ameeleza kuwa kwa mwaka wa fedha 2018/2019 jumla ya mikopo yenye thamani ya Tsh. 51,744,000/= na ilitolewa kwa vikundi 13 vya wanawake, 4 vijana na 3 walemavu vikiwa na jumla ya wanufaika 307. Kuanzia mwaka wa fedha 2019/2020 hadi kufikia disemba 2019 jumla ya mkopo wa Tsh. 32,950,000/= umetolewa ambapo vikundi 9 vya wanawake wamekabidhiwa Tsh. 24,250,000/=, kikundi 1 cha vijana Tsh 5,700,000/= na kikundi kimoja cha walemavu Tsh 3,000,000/=.

Zoezi la ugawaji wa fedha hizo limefanyika katika ukumbi mkubwa wa Halmashauri ambapo palitanguliwa na kikao cha Baraza hilo ambao waheshimiwa madiwani wamejadili taarifa za robo ya pili yani septemba hadi disemba.

Aidha Maduhu amelieleza baraza la madiwani kuwa Wilaya ya Ukerewe inategemea kupokea boti ya wagonjwa wa dharura ambapo majaribio ya boti hiyo yameshafanyika na boti inatarajiwa kufika wilayani Ukerewe hivi karibuni. Boti ya wagonjwa wa dharura (ambulance boat) itakuwa inabeba wagonjwa kutoka visiwani kupelekwa Hospitali ya Wilaya Ukerewe na Mwanza kwa matibabu yakibingwa.

Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JKT- UKEREWE January 22, 2026
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA MILIONI 9O6.9

    January 19, 2026
  • MFUMO WA SIS KUONGEZA UFANISI SHULENI

    January 14, 2026
  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.