• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

WAVUVI UKEREWE KUANZA KUNUFAIKA NA VYAMA VYA USHIRIKA

Posted on: September 24th, 2019

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi  Mhe. Abdallah Ulega amefanya ziara ya siku moja katika vijiji vya Malelema kata ya Bukungu kisiwani Ukara na Musozi kata ya Bukindo Wilayani Ukerewe.  Lengo ikiwa ni kusikiliza changamoto za kiuchumi zinazowakumba katika sekta hizo vijijini humo.

Akizungumza kwenye mkutano huo Mhe. Ulega alianza kwa kutoa pole kwa wananchi wa Wilaya ya Ukerewe hasa wa kisiwa cha Ukara kutokana na ajali ya MV Nyerere iliyotokea tarehe 20 mwezi Septemba 2018, ikitimiza mwaka mmoja tangu kutokea kwa ajali hiyo. Pia alitoa pongezi kwa Wananchi kwa kuwa na Viongozi wazuri akitolea mfano Mhe. Pius Msekwa, aliyewahi kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Vilevile amewapongeza Wananchi wa kijiji cha Malelema kisiwa cha Ukara kwa kuwa mstari wa mbele kupinga Uvuvi haramu.

Wakielezea baadhi ya changamoto kubwa katika sekta ya uvuvi wananchi wa kijiji cha Malelema wanakabiliwa na sintofahamu kuhusu mipaka ya ziwa Victoria baina ya Tanzania na Uganda ikiwa ndo ziwa pekee linalotumika katika shughuli ya Uvuvi. Vilevile wameeleza mkanganyiko juu ya Zana sahihi zinazofaa kwa ajili ya Uvuvi.

Akijibu hoja ya Zana sahihi za Uvuvi,  Afisa Uvuvi Wilaya ya Ukerewe ndugu Abbubakar Murshid amesema ndoano namba 1, 2, na 3, zinaruhusiwa kutumia kwa ajili ya shughuli za Uvuvi, namba 4, 5, 6, na 7 haziruhusiwi  kabisa, pia namba 9, 10, 11, 12 na kuendelea zinaruhusiwa maeneo tengefu.  

Mhe. Ulega  akijibu hoja za wananchi amesema, suala la kuhusu mipaka Wizara italifanyia kazi, pia ametoa  agizo la mwezi mmoja kwa wananchi kuunda vyama Ushirika ili kuweza kurahisisha upatikanaji wa  mikopo kutoka Taasisi za kifedha, kama vile Benki na Vikundi mbalimbali. Aidha amezungumzia bado utafiti unafanyika  kuhusu matumizi ya nishati ya juu (solar) katika shughuli ya uvuvi  hivyo wavuvi waendelee kutumia taa za mafuta.

Halikadhalika ametoa agizo josho la mifugo katika kijiji cha Musozi kufanyiwa marekebisho na kuahidi kiasi cha shilingi milioni mbili (2,000,000) kama kianzio cha marekebisho hayo. Pia amesisitiza kushughulikia suala la kuongeza wataalamu wa mifugo ili wananchi kuweza kupata huduma staiki. Vilevile amepokea ombi la mfumo wa ukopeshaji wa mifugo uliojulikana kama “kopa ng’ombe lipa ngo’mbe”  uliokuwepo hapo awali.

Akihitimisha mkutano katika kijiji cha Malelema kisiwani Ukara, Mhe. Cornell Magembe Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, amesisitiza wananchi kuhudhuria vikao mbalimbali vinavyo itishwa  na viongozi wa serikali kwa ajili ya maendeleo ya jamii kwa  ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 July 20, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI ZA UDEREVA HALMASHAURI YA WILAYA UKEREWE July 23, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WAKUSANYA MAPATO July 27, 2022
  • TAARIFA YA UTOAJI WA MIKOPO YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU ROBO YA NNE August 03, 2022
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru wakabidhiwa salama wakabidhiwa salama wilaya ya ILemela .

    July 16, 2023
  • Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Col. Deniss F. Mwila atia saini Mkataba wa utekelezaji wa Afua za Lishe utakaotekelezwa wilaya ya Ukerewe.

    October 28, 2022
  • MAKUBALIANO YA UJENZI WA KIWANDA KIDOGO CHA BARAFU WILAYA YA UKEREWE

    October 09, 2022
  • UZINDUZI WA VITABU VYA MAELEKEZO YA JINSI YA KUBORESHA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI WILAYA YA UKEREWE.

    September 08, 2022
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.