• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Ukerewe District Council
Ukerewe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
        • Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
        • Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Ugavi na Manunuzi
      • Utamaduni ,sanaa na michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Maji
    • Uvuvi
    • Kilimo na Umwagiliaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyoidhinishwa
    • Ongoing Projects
    • Miradi Iliyo kamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Sheria Ndogondogo za Halmashauri
    • Fomu za Maombi
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba za Viongozi
    • Taarifa kwa Umma
    • Video

ZAO LA KAHAWA NGUZO YA PILI YA UCHUMI UKEREWE

Posted on: November 11th, 2025

".. tuondokane na fikra za zamani na mazoea juu ya uwekezaji katika eneo la uvuvi tu tuitumie ardhi pia, tulifanye zao la kahawa kuwa nguzo ya pili ya uchumi wetu. Serikali imeweka nguvu kubwa katika zao hili ili kuongeza ajira kwa vijana na kipato kwa wananchi wa Ukerewe .." 

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Ukerewe Cde, Christopher Ngubiagai katika hafla ya ugawaji wa miche ya zao la kahawa katika kijiji cha Busagami kata ya Namilembe ambapo jumla ya miche 26,000 imegawiwa kwa vyama vya ushirika (AMCOS) 14 vilivyopo wilayani Ukerewe.

Aidha Cde, Ngubiagai amesema maendeleo ya kweli hayaji kwa maneno bali kwa vitendo, amewataka wananchi kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kilimo kwa kulienzi zao hilo na kulisimamia ili kukuza uchumi huku akiweka wazi ujio wa miche mingine zaidi ya laki nne katika wilaya ya Ukerewe.

 Nae Mwenyekiti wa Nyanza Cooperative Union (NCU) ndugu Leonard Lyabalima amesema kahawa ina uwezo mkubwa wa kubadilisha maisha ya wanaukerewe nakuiomba serikali kuwapa kipaumbele wakulima wa zao hilo na kuahidi kutoa ushirikiano mkubwa kwa wakulima.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ukerewe ndugu Wanchoke Chinchibela amesema Halmashauri itakuwa bega kwa bega na wakulima wote na kuwaagiza maafisa ugani kuendelea kusimamia  na kutoa elimu juu ya ustawi wa miche hiyo.

Mkufunzi na mzalishaji wa kahawa Bi. Amina Yusuph Kashoro amewataka wakulima kulinda miche yao kwa kuzingatia mahitaji yote kama mbolea na kumwagilizia maji kwa vipindi na kuwa waangalifu wa mifugo ili kufaidi matunda ya kilimo cha zao hilo.

Ernest Andrew Goroba ni mwanachama wa AMCOS Nduruma yeye amepongeza jitihada za serikali kurejesha zao hilo lililowanufaisha zamani huku akiwaomba wana ukerewe kulipokea kwa mikono miwili ili kuijenga kesho bora ya Ukerewe.

Cde, Ngubiagai amehitimisha hafla hiyo kwa kutoa rai kwa wana ukerewe wote kuijenga Ukerewe ya kijani kupitia zao la kahawa na kuahidi ushirikiano wa moja kwa moja kwa wakulima wote ili kujenga mazingira rafiki ya kilimo cha biashara wilayani humo.



















Matangazo

  • NAMNA YA KUOMBA LESENI ZA BIASHARA KUPITIA MFUMO WA TAUSI September 17, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JKT- UKEREWE January 22, 2026
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • DC NGUBIAGAI ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA MILIONI 9O6.9

    January 19, 2026
  • MFUMO WA SIS KUONGEZA UFANISI SHULENI

    January 14, 2026
  • WANAFUNZI WASIZUILIWE KUJIUNGA NA SHULE KWA KUKOSA MAHITAJI

    January 08, 2026
  • UKEREWE DC YAZIDI KUJIDHATITI UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    January 06, 2026
  • Angalia Zaidi

Video

FURSA ZA UWEKEZAJI UKEREWE
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • https://www.moe.go.tz/sw/article/tangazo-la-nafasi-za-mafunzo-ya-ualimu-ngazi-ya-astashahada-ya-ualimu-elimu-ya-awali-msingi-na-stashahada-ya-ualimu-elimu-sekondari-sayansi-miaka-mitatu-kwa-mwaka-wa-masomo-20222023
  • Jiwe linalocheza Wilayani Ukerewe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Necta

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2022 Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe . All rights reserved.